Kutoka 17:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
9 Musa akamwambia Yoshua: “Chagua wanaume uende upigane na Waamaleki. Kesho nitasimama juu ya kilele cha kilima, nikishika katika mukono wangu ile fimbo ya Mungu.”
Lakini juu ya mambo mengine, chagua kati ya watu wote, watu wanaostahili, watu wanaomwogopa Mungu, waaminifu na wanaochukia kituliro. Uwape hao mamlaka, wakuwe na kazi ya kuwasimamia watu katika makundi ya watu elfu, mia, makumi tano na kumikumi.
Hivi ndivyo Yawe alivyokuwa akiongea na Musa uso kwa uso, kama mutu na rafiki yake. Kisha Musa alirudi tena katika kambi. Naye kijana Yoshua mwana wa Nuni ambaye alikuwa mutumishi wake hakuondoka ndani ya hema.
Basi, Musa akatwaa muke wake na watoto wake, akawapandisha juu ya punda, akaanza safari ya kurudi Misri. Katika mukono wake alishika ile fimbo aliyoamuriwa na Mungu aitwae.
Kisha ile hema ikaachwa kwa kizazi cha babu zetu kilichofuata. Nao wakaibeba chini ya uongozi wa Yoshua mpaka waliponyanganya inchi ya mataifa yale Mungu aliyofukuza mbele ya kufika kwao. Nayo ikabaki katika inchi mpaka katika siku za Daudi.
Halafu Yawe akamwambia Yoshua: “Elekeza mukuki wako kule katika muji wa Ai maana nitautia muji ule katika mikono yako.” Yoshua akaelekeza mukuki wake kwenye muji wa Ai.