Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Kutoka 17:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Pahali pale Musa akapaita “Masa” na “Meriba”, ni kusema “Ujaribu” na “Magombano”, kwa sababu Waisraeli walimugombanisha na kumujaribu Yawe wakisema: “Kweli Yawe yuko pamoja nasi?”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Kutoka 17:7
21 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Walimukasirikisha Mungu penye maji ya Meriba. Musa akapata taabu kwa ajili yao.


Walimujaribu Mungu kwa makusudi; wakidai wapewe chakula walichotaka.


“Mimi nilikutua mizigo yako toka kwenye mabega, nilikuondolea matofali uliyochukua katika mikono.


Katika shida uliniita, nami nikakuokoa. Nilikujibu kutokea katika ngurumo. Nilikujaribu kwenye maji ya Meriba.


“Musikuwe wagumu kama kule Meriba, kama ilivyokuwa kule Masa katika jangwa,


Kwa hiyo watu wakamunungunikia Musa wakisema: “Utupatie maji ya kunywa.” Musa akawauliza: “Mbona munaninungunikia? Mbona munamujaribu Yawe?”


Kisha akasema: Ee Bwana wangu, kama nimepata kukubaliwa mbele yako, ninakuomba uende pamoja nasi. Watu hawa ni wenye vichwa vigumu, lakini utusamehe uovu wetu na zambi yetu, utupokee kama watu wako mwenyewe.


Mupige vigelegele na kuimba kwa furaha, enyi wakaaji wa Sayuni, maana Mutakatifu wa Israeli ni makubwa kati yenu.


Waamuzi wanahukumu kwa kupewa kutuliro, makuhani wake wanafundisha kwa kupata malipo, manabii wanatabiri kwa kupata feza. Hata hivyo wanajidai kumutegemea Yawe, wakisema: Yawe, si yupo pamoja nasi? Hatutapatwa na hasara yoyote!


hakuna hata mumoja wao ambaye amekwisha kuuona utukufu wangu na vitambulisho vyangu nilivyofanya Misri na katika jangwa kisha akazidi kunijaribu mara hizi zote bila ya kutii sauti yangu,


Hayo ni maji ya Meriba, ni kusema ya “Magombano”, pahali ambapo Waisraeli walimugombanisha Yawe, naye akajionyesha kwa utakatifu kati yao.


Haruni atakufa; hataingia katika inchi ambayo nimewapa Waisraeli kwa sababu ninyi wawili muliasi amri yangu kule Meriba.


kwa sababu hamukuitii amri yangu kule katika jangwa la Sini, wakati watu wote pamoja waliponigombanisha kule Meriba. Ninyi hamukuacha utukufu wangu uonekane mbele yao walipotaka wapewe maji. (Meriba ni chemichemi ya maji ya Kadesi katika jangwa la Sini).


Neno alifanywa kuwa mutu, naye akaishi kati yetu, akijaa neema na ukweli. Tuliona utukufu wake, utukufu ule Mwana wa pekee aliopewa na Baba.


Hapo hasira yangu itawawakia siku hiyo, nami nitawaacha na kuficha uso wangu mbali nao, wataangamizwa. Maovu mengi na taabu zitawapata hata watambue kwamba maovu hayo yamewapata kwa sababu Mungu wao hayuko kati yao.


Juu ya kabila la Lawi, akasema: “Ee Yawe, upatie wazao wa Lawi shauri lako, shauri lako kwa hao waaminifu wako, ambao uliwajaribu huko Masa. Ulishindana nao kwenye maji ya Meriba.


“Musimujaribu Yawe, Mungu wenu, kama vile mulivyomujaribu huko Masa.


“Tena mulimukasirikisha Yawe, Mungu wenu, huko Tabera, Masa na Kiburoti-Hatawa.


Naye Finehasi mwana wa kuhani Eleazari, akayaambia makabila ya Rubeni na Gadi na nusu ya kabila la Manase: “Leo tumejua kwamba Yawe yuko kati yenu maana hamukumufanyia Mungu uasi. Sasa mumewaokoa Waisraeli wasiazibiwe na Yawe.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ