Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Kutoka 17:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Angalia mimi nitasimama mbele yako juu ya jiwe la mulima wa Horebu, nawe utapiga lile jiwe na maji yatabubujika kutoka mule kusudi watu wote wapate kunywa.” Basi, Musa akafanya hivyo mbele ya wazee wa Waisraeli.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Kutoka 17:6
24 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Walipokuwa na njaa, ukawapa chakula kutoka mbinguni. Walipokuwa na kiu, ukawapa maji kutoka katika jiwe. Ukawaagiza kurizi inchi uliyokuwa umewaahidi.


Alipasua jiwe maji yakabubujika; yakatiririka katika jangwa kama muto.


anayegeuza jiwe kubwa kuwa ziwa, nalo jiwe gumu kuwa chemichemi za maji!


hata kama bahari ikichafuka na kutisha, na milima ikitetemeka kwa machafuko yake.


Wewe umefanya chemichemi na vijito; na kukausha mito mikubwa.


Walimujaribu Mungu kwa makusudi; wakidai wapewe chakula walichotaka.


Ni kweli, alipiga jiwe, maji yakatiririka kama muto; lakini, sasa anaweza kweli kutupatia mukate, na kuwapatia watu wake nyama?”


“Mimi nilikutua mizigo yako toka kwenye mabega, nilikuondolea matofali uliyochukua katika mikono.


Inua fimbo yako na kuielekeza juu ya bahari. Maji yatagawanyika na Waisraeli wataweza kuvuka katikati ya bahari pahali pakavu.


Wakati Haruni alipokuwa akizungumuza na Waisraeli wote pamoja, watu wote wakaangalia kule katika jangwa na mara moja utukufu wa Yawe ukaonekana katika mawingu.


Alipowaongoza katika jangwa hawakuona kiu, aliwatiririshia maji kutoka katika jiwe, alipasua jiwe maji yakabubujika.


Twaa ile fimbo yako, kisha wewe na ndugu yako Haruni mukusanye watu wote pamoja. Halafu, mbele ya macho yao, uambie jiwe linalokuwa mbele ya macho yao litoe maji yake. Utawatoshea maji ndani ya jiwe watu wote na mifugo yao waweze kunywa.


Yesu akamujibu: “Kama ungejua kitu Mungu anachoweza kukupatia, na ni nani anayekuomba maji ya kunywa, wewe ndiwe ungemwomba, naye angekupa maji ya uzima.”


lakini yeyote atakayekunywa maji yale nitakayomupa, hatasikia kiu tena hata kidogo. Maji nitakayomupa yatakuwa ndani yake kama chemichemi inayotiririka maji ya uzima wa milele.”


Wote walikunywa kinywaji kimoja cha kiroho; kwa maana walikunywa maji yaliyotoka ndani ya lile jiwe lililosafiri pamoja nao, nalo jiwe lilikuwa Kristo.


(Ni mwendo wa siku kumi na moja kutoka mulima Horebu mpaka Kadesi-Barnea kwa njia ya mulima Seiri.)


Ni yeye aliyewaongoza katika lile jangwa kubwa na la kutisha, lenye nyoka wenye sumu na nge katika inchi ile yenye kukauka isiyokuwa na maji, aliwatolea maji kutoka kwenye jiwe gumu.


Roho na Bibi arusi wanasema: “Kuja!” Naye mwenye kusikia maneno haya aseme vilevile: “Kuja!” Yule anayesikia kiu akuje, na yule anayetaka maji ya uzima akuje kuyapokea kwa bure.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ