Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Kutoka 17:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Kwa hiyo watu wakamunungunikia Musa wakisema: “Utupatie maji ya kunywa.” Musa akawauliza: “Mbona munaninungunikia? Mbona munamujaribu Yawe?”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Kutoka 17:2
32 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Lakini bila kukawia walisahau matendo yake, wakaacha kutegemea shauri lake.


Walipatwa na tamaa kubwa kule katika jangwa, wakamupima Mungu kule kwenye ukiwa.


Walimujaribu Mungu kwa makusudi; wakidai wapewe chakula walichotaka.


Walimujaribu Mungu tena na tena, wakamukasirikisha huyo Mutakatifu wa Israeli.


Hata hivyo walimupima na kumwasi Mungu Mukubwa; wala hawakushika maagizo yake.


“Musikuwe wagumu kama kule Meriba, kama ilivyokuwa kule Masa katika jangwa,


babu zenu waliponijaribu na kunipima, ingawa walikuwa wameona mambo niliyowatendea.


Basi, watu wote wakamunungunikia Musa wakisema: “Sasa tutakunywa nini?”


Tena Musa akasema: “Magaribi, Yawe atawapa nyama mupate kula na asubui atawapa mikate mupate kula na kushiba. Maana yeye ameyasikia manunguniko muliyomunungunikia. Sisi ni nani hata mutunungunikie? Musitunungunikie sisi lakini mumunungunikie Yawe.”


Pahali pale Musa akapaita “Masa” na “Meriba”, ni kusema “Ujaribu” na “Magombano”, kwa sababu Waisraeli walimugombanisha na kumujaribu Yawe wakisema: “Kweli Yawe yuko pamoja nasi?”


Basi, wakawaambia Musa na Haruni: “Yawe aone jambo hili na kuwahukumu ninyi kwa sababu mumetufanya sisi kuwa chukizo kwa mufalme wa Misri na wakubwa wake. Ninyi mumewapa sababu ya kutuua.”


Ahazi akajibu: Sitaomba kitambulisho! Sitaki kumujaribu Yawe.


Tunayoona sisi, ni kwamba wenye kiburi ndio wenye furaha siku zote. Watu waovu, ingawa wanastawi, hata wanapomujaribu Mungu, hawapati azabu.


Wakamunungunikia Musa na Haruni wakisema: Afazali tungekufia Misri! Afazali tungekufia hapahapa katika jangwa!


hakuna hata mumoja wao ambaye amekwisha kuuona utukufu wangu na vitambulisho vyangu nilivyofanya Misri na katika jangwa kisha akazidi kunijaribu mara hizi zote bila ya kutii sauti yangu,


Basi, wakaanza kumunungunikia Mungu na Musa, wakisema: Kwa nini mumetutoa Misri tukuje tukufie humu katika jangwa? Humu hamuna chakula wala maji; nasi tumechokeshwa na chakula hiki cha bure.


Yesu akamujibu: “Imeandikwa hivi vilevile: ‘Usimujaribu Bwana Mungu wako.’ ”


Yule mudogo akamwambia baba yake: ‘Baba, unipe ile sehemu ya urizi inayopaswa kuwa yangu.’ Basi baba akagawanya mali yake kati ya wana wake wote wawili.


Lakini Yesu akamujibu: “Imeandikwa katika Maandiko Matakatifu: ‘Usimujaribu Bwana Mungu wako.’ ”


Basi sasa, kwa nini munataka kumupima Mungu kwa kuwabebesha muzigo ambao wala babu zetu, wala sisi wenyewe hatukuweza kuubeba?


Halafu Petro akamwambia: “Namna gani mulipatana kwa kumupima Roho wa Bwana? Sikiliza! Wale wanaotoka kumuzika mume wako wamefika hapa kwenye mulango, nao watakupeleka vilevile.”


Vilevile tusimupime Bwana kama vile wamoja wao walivyofanya, hata wakauawa na nyoka.


“Musimujaribu Yawe, Mungu wenu, kama vile mulivyomujaribu huko Masa.


“Tena mulimukasirikisha Yawe, Mungu wenu, huko Tabera, Masa na Kiburoti-Hatawa.


Kule babu zenu walinipima na kunijaribia, ingawa walikuwa wameona yote niliyotenda kwa muda wa miaka makumi ine.


Lakini jambo la Waisraeli la kutaka wapewe mufalme wa kuwatawala, halikumupendeza Samweli. Naye akamwomba Yawe.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ