Tena Musa akasema: “Magaribi, Yawe atawapa nyama mupate kula na asubui atawapa mikate mupate kula na kushiba. Maana yeye ameyasikia manunguniko muliyomunungunikia. Sisi ni nani hata mutunungunikie? Musitunungunikie sisi lakini mumunungunikie Yawe.”
Pahali pale Musa akapaita “Masa” na “Meriba”, ni kusema “Ujaribu” na “Magombano”, kwa sababu Waisraeli walimugombanisha na kumujaribu Yawe wakisema: “Kweli Yawe yuko pamoja nasi?”
Basi, wakawaambia Musa na Haruni: “Yawe aone jambo hili na kuwahukumu ninyi kwa sababu mumetufanya sisi kuwa chukizo kwa mufalme wa Misri na wakubwa wake. Ninyi mumewapa sababu ya kutuua.”
hakuna hata mumoja wao ambaye amekwisha kuuona utukufu wangu na vitambulisho vyangu nilivyofanya Misri na katika jangwa kisha akazidi kunijaribu mara hizi zote bila ya kutii sauti yangu,
Basi, wakaanza kumunungunikia Mungu na Musa, wakisema: Kwa nini mumetutoa Misri tukuje tukufie humu katika jangwa? Humu hamuna chakula wala maji; nasi tumechokeshwa na chakula hiki cha bure.
Yule mudogo akamwambia baba yake: ‘Baba, unipe ile sehemu ya urizi inayopaswa kuwa yangu.’ Basi baba akagawanya mali yake kati ya wana wake wote wawili.
Halafu Petro akamwambia: “Namna gani mulipatana kwa kumupima Roho wa Bwana? Sikiliza! Wale wanaotoka kumuzika mume wako wamefika hapa kwenye mulango, nao watakupeleka vilevile.”