Beni-Hadadi akamutumia Ahabu ujumbe huu: “Miungu iniue ikiwa kule Samaria kutabakia mavumbi ya kutosha kwa kujaza vitanga vya mikono kwa kila mumoja wa watu wangu wengi wanaonifuata!”
Mufalme wa Misri aliposikia kwamba Waisraeli wamekimbia, yeye na wakubwa wake walibadilisha mafikiri yao, wakasema: “Tumefanya nini kwa kuwaachilia Waisraeli waende zao wasitutumikie tena?”
Kwa hiyo nitamugawanyia sehemu pamoja na wakubwa, atagawanya vitu vilivyotekwa pamoja na wenye nguvu. Alijitoa yeye mwenyewe hata kufa; aliwekwa kundi moja na watu wakosaji. Alizibeba zambi za watu wengi, akawaombea musamaha hao wakosaji.
Lakini mutu mwingine mwenye nguvu zaidi akimushambulia na kumushinda, anamunyanganya silaha zake alizotegemea na kugawanya vitu vya unyanganyi anavyokuwa navyo.
‘Bila shaka wanatafuta na kugawanyana vitu: binti mumoja au wawili kwa kila askari, nguo ya sufu ya rangi kwa ajili ya Sisera, nguo ya sufu iliyopindwa vizuri, na mikufu miwili yenye kufumwa kwa ajili ya shingo yangu!’