Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Kutoka 15:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Kwa wingi wa ukubwa wako unawaangamiza wapinzani wako; unawapulizia kasirani yako nayo inawateketeza kama maganda.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Kutoka 15:7
29 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yeye ni mwenye hekima sana na nguvu nyingi. Nani aliyepingana naye, akashinda?


Wote musifu jina la Yawe, maana jina lake peke yake linatukuzwa; utukufu wake unapita dunia na mbingu.


Wao wanatenda zambi katika masemi yao yote, kwa hiyo wanaswe katika kiburi chao! Kwa sababu ya laana na uongo wao,


Enyi falme za dunia, mumwimbie Mungu, mumwimbie Bwana wetu nyimbo za sifa,


ambao walisema: “Tutajitwalia inchi ya Mungu.”


Basi, Musa akanyoosha mukono wake juu ya bahari na kulipopambazuka bahari ikarudilia hali yake ilivyokuwa. Wamisri wakajaribu kukimbia maji lakini Yawe akawasukumizia ndani ya bahari.


Basi, watu wote wakatawanyika kila pahali katika inchi ya Misri wakitafuta nyasi za kutengeneza matofali.


Lakini nimewaacha muishi kwa kuonyesha uwezo wangu. Kwa hiyo dunia yote itatambua kwamba mimi ni nani.


Ee, Yawe, fungua macho uone, tega sikio lako uyasikie matusi yote ambayo Saniharibu amepeleka na kukutukana wewe Mungu Mwenye Uzima.


Wewe umemutukana nani? Umemutusi nani? Umesubutu kumufokea nani kwa majivuno? Ni Mungu, Mutakatifu wa Israeli!


Kwa vile umefanya mipango juu yangu na nimesikia majivuno yako, nitatia ndoana yangu ndani ya pua yako, na lijamu yangu ndani ya kinywa chako. Nitakurudisha katika njia ileile uliyokuja ndani yake.


Basi, malaika wa Yawe aliingia ndani ya kambi ya Waasuria na kuwaua watu elfu mia moja makumi nane na watano. Kesho yake, wakati watu walipoamuka, waliona yale maiti yote.


Siku moja, wakati Saniharibu alipokuwa akiabudu katika nyumba ya Nisiroki mungu wake, wana wake wawili, Adarameleki na Sarezeri, walimwua kwa upanga, halafu wakakimbilia katika inchi ya Ararati. Halafu mwana wake Esari-Hadoni akatawala kwa pahali pake.


Wao ni kama majani yenye kukauka: moto utayateketeza! Hawawezi hata kujiokoa wenyewe mbali na ukali wa moto huo. Moto huo si wa kujipatia joto, huo si moto wa kuota!


Lakini Yawe wa majeshi anatukuzwa wakati sheria yake inafuatwa. Utakatifu wa Mungu Mutakatifu unaonyeshwa wakati haki inatendwa.


Kwa hiyo, kama vile moto unavyoteketeza nyasi, kama vile majani yanavyotoweka ndani ya moto, ndivyo mizizi yao itakavyooza, na maua yao yatakavyopeperushwa juu kama mavumbi. Maana wameacha sheria ya Yawe wa majeshi, wamezarau neno la yule Mutakatifu wa Israeli.


Ee Yawe, hakuna anayekuwa kama wewe; wewe ni mukubwa na nguvu yako inajulikana.


Mataifa mengi yamekusanyika kwa kuwashambulia. Yanasema: Muache muji wao uchafuliwe, nasi tufurahie kuona uharibifu wa Sayuni!


Kisha Yawe atatoka na kuyapiga vita mataifa hayo, kama vile anavyofanya siku zote wakati wa vita.


Wakati ule, maji ya uzima yatabubujika kutoka Yerusalema, na nusu ya maji yale yatatiririkia kwenye bahari ya mashariki, na nusu ingine kwenye bahari ya magaribi. Maji yale yataendelea kububujika wakati wa kipwa kama yanavyokuwa wakati wa mvua.


Basi, huyo malaika aliyezungumuza nami akamwambia yule mwenzake: Kimbia umwambie yule kijana kwamba si lazima Yerusalema ukuwe na kuta, kama sivyo hapatakuwa nafasi ya kuwatoshelea wakaaji wake wengi na nyama watakaokuwa ndani yake.


Yeye anashika lungo katika mikono yake kwa kupepeta ngano. Atakusanya ngano na kuitia katika gala yake, lakini atateketeza maganda katika moto usiozimika.”


Akaanguka chini, akasikia sauti ikimwambia: “Saulo, Saulo, sababu gani unanitesa?”


Musa akamalizia kwa kusema: “Ee Israeli, hakuna anayekuwa kama Mungu wako, yeye anayeruka toka mbinguni kuja kukusaidia, anapita juu katika anga katika utukufu wake.


maana Yawe, Mungu wenu, ni moto unaoteketeza. Yeye ni Mungu mwenye wivu.


kwa maana Mungu wetu ni kama moto wenye kuteketeza.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ