Uligawanya bahari katikati mbele yao, nao wakapita katikati ya bahari, pahali pakavu. Lakini ukawatupa Wamisri waliowafuatilia kama jiwe zito ndani ya maji mengi.
Maji yakafunika magari pamoja na wapanda-farasi. Jeshi lote la mufalme wa Misri lililokuwa limewafuatilia Waisraeli likakufa katika bahari. Hakukuponyoka Mumisri hata mumoja.
Kitisho na hofu vimewashika. Kwa sababu ya ukubwa wa nguvu zako, wao wamenyamaza kimya kama jiwe, mpaka watu wako, ee Yawe, wapite, mpaka watu wale uliowakomboa wamewapita.
Kisha malaika mumoja mwenye uwezo akanyanyua jiwe linalokuwa kama jiwe kubwa la kusagia. Akalitupa katika bahari akisema: “Ni hivi muji mukubwa wa Babeli utakavyotupwa kwa nguvu, nao hautaonekana tena.