Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Kutoka 15:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Yawe ananijalia nguvu na uwezo, yeye mwenyewe ndiye anayeniokoa. Yeye ni Mungu wangu nami nitamusifu; ni Mungu wa baba yangu nami nitamutukuza.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Kutoka 15:2
64 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

“Nitasimamisha agano langu nawe, wazao wako na vizazi vyao vyote milele; nitakuwa Mungu wako na Mungu wa wazao wako milele.


Mungu wangu, yule ambaye ninamukimbilia, ngao yangu, nguvu ya wokovu wangu, munara wangu, kimbilio langu. Mwokozi wangu, unaniokoa kutoka watesaji wakali!


Yawe anaishi! Asifiwe yeye kikingio changu! Atukuzwe Mungu, kikingio na mwokozi wangu.


Mungu anamujalia mufalme wake ushindi mukubwa; anamutendea mema muchaguliwa wake, ndiye Daudi na wazao wake milele.


Hata umewaimarisha watu wako Waisraeli kwa ajili yako mwenyewe, kusudi wakuwe watu wako milele; nawe ee Yawe umekuwa Mungu wao.


“Kwenda umwambie mutumishi wangu Daudi: Yawe anasema hivi: Si wewe utakayenijengea nyumba ya kukaa.


Hakika, nimekujengea nyumba ya kukaa, pahali pa makao yako ya milele.”


“Lakini, ee Mungu, kweli utakaa katika dunia? Ikiwa hata mbingu zenyewe wala mbingu za juu sana hazikutosha, namna gani nyumba hii ambayo nimeijenga itakutoshelea?


Yeye Yawe, ndiye Mungu wetu; hukumu zake zina nguvu katika dunia yote.


Kwa mukubwa wa waimbaji. Wimbo wa Daudi. Usinyamaze, ee Mungu, ninayekusifu!


Yawe ni nguvu yangu kubwa; yeye mwenyewe ndiye wokovu wangu.


Ninakushukuru, ee Yawe, kwa kunijibu; kwa sababu wewe ni wokovu wangu.


Wewe ni Mungu wangu, ninakushukuru; ninakutukuza, ee Mungu wangu.


mpaka nikutayarishie wewe Yawe nafasi ya kukaa, ndiyo makao yako, ewe Mwenye Nguvu wa Yakobo!”


Ninamwambia Yawe: “Wewe ni Mungu wangu.” Usikilize, ee Yawe, sauti ya ombi langu.


Wimbo wa sifa wa Daudi. Nitakutukuza, ee Mungu wangu na mufalme wangu; nitalitukuza jina lako kwa milele na milele.


Wageni walivunjika moyo; wakakuja kutoka makimbilio yao wakitetemeka.


Lakini wewe ndiwe uliyenitoa katika tumbo la mama yangu, uliniweka salama kwa kifua cha mama yangu.


Ee Mungu wangu, ninakulilia muchana lakini haujibu; ninakulalamikia usiku, lakini sipumziki.


Zaburi ya Daudi. Yawe ni mwangaza wangu na wokovu wangu, ni nani nitakayemwogopa? Yawe ni mulinzi wa maisha yangu, sitamwogopa mutu yeyote.


Yawe ni nguvu ya watu wake; yeye ni kimbilio la mufalme aliyemuchagua.


Mashairi yanayoelekea muzinduo wa hekalu. Zaburi ya Daudi.


Mimi nitajisifu kwa ajili ya Yawe; wanyenyekevu wasikie na kufurahi.


Muangalie kuta zake na kuchunguza pango zake za kukimbilia, mupate kuelezea vizazi vitakavyokuja kwamba:


Lakini mimi nitaimba sifa za nguvu yako, nitashangilia asubui juu ya wema wako, maana wewe umekuwa kikingio changu, wewe ni kimbilio langu wakati wa taabu.


Yawe asifiwe siku kwa siku! Yeye anatubebea mizigo yetu, yeye ndiye Mungu mwokozi wetu.


Mumusifu Yawe, Mungu wetu; muiname uso mpaka chini mbele yake. Yeye ni mutakatifu!


Mumusifu Yawe, Mungu wetu; muiname kwa mulima wake mutakatifu! Yawe, Mungu wetu, ni mutakatifu.


Musa akawaambia Waisraeli: “Musiogope! Musimame imara! Leo mutaona jinsi Yawe atakavyowaokoa. Maana, hawa Wamisri munaowaona leo, hamutawaona tena.


Kisha Mungu akamwambia: “Mimi ni Mungu wa baba yako, Mungu wa Abrahamu, Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo.” Musa akafunika uso wake kwa sababu aliogopa kumwangalia Mungu.


Nawe utamwambia mufalme wa Misri kwamba Yawe anasema hivi: ‘Israeli ni mwana wangu, muzaliwa wangu wa kwanza.


Kisha, lile wingu likafunika lile hema la mukutano na utukufu wa Yawe ukajaza hema.


Nitawafanya kuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wenu. Ninyi mutatambua kwamba mimi ni Yawe, Mungu wenu, niliyewatoa katika nira za Wamisri.


Mungu ndiye mwenye kuniokoa, nitamutegemea yeye, wala sitaogopa; Yawe ananijalia nguvu; yeye mwenyewe ndiye anayeniokoa.


Wewe, ee Yawe, ndiwe Mungu wangu; nitakutukuza na kulisifu jina lako, kwa maana umetenda mambo ya ajabu; unaitimiza kwa uaminifu na kweli mipango uliyoipanga tangu zamani.


Lakini taifa la Israeli litaokolewa na Yawe, litapata wokovu wa milele. Halitapata haya wala kuzarauliwa milele.


Yeye anasema: Haitoshi tu wewe kuwa mutumishi wangu, kusudi uyainue makabila ya Yakobo, na kurudisha watu wa Israeli waliobaki. Nitakufanya ukuwe mwangaza wa mataifa, kusudi watu wote wapate kuokolewa katika dunia.


Yawe anasema hivi: Mbingu ni kiti changu cha kifalme, dunia ni kiti cha kupumzikishia miguu yangu. Mutanijengea nyumba ya namna gani basi, pahali nitakapoweza kupumzikia?


Kweli tumedanganyika sana kwa kutambikia huko kwenye vilima, hakika wokovu wa Israeli unatoka kwake Yawe, Mungu wetu.


Kisha siku hizo, nitafanya agano hili na Waisraeli. Nitaiweka sheria yangu ndani yao, na kuiandika katika mioyo yao. Mimi nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu. Ni mimi Yawe ninayesema hivyo.


Nao watakuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wao.


Ulitoka kwenda kuwaokoa watu wako, kumwokoa yule uliyemusimika kwa kumupakaa mafuta. Ulimuponda mutawala wa jamii ya waovu, ukawaangamiza kabisa wafuasi wake.


Sehemu hiyo moja ya tatu itakayobaki, nitaipima na kuitakasa, kama vile mutu anavyosafisha feza, kama vile wanavyopima zahabu. Halafu wao wataniomba mimi, nami nitawajibu. Nitasema: Hawa ni watu wangu, nao watasema: Yawe, ndiye Mungu wetu.


Upate kuwajulisha watu wake kwamba atawaokoa akisamehe zambi zao.


Nimejionea mwenyewe wokovu unaotoka kwako,


Ninyi Wasamaria hamujui munachokiabudu; sisi tunajua tunachokiabudu kwa sababu wokovu unatokea kwa njia ya Wayuda.


kusudi watu wote wamuheshimu Mwana kama vile wanavyomuheshimu Baba. Asiyemuheshimu Mwana, hamuheshimu Baba aliyemutuma.


“Hivi hakuna anayeweza kuokolewa kwa njia ya mutu mwingine yeyote, kwa maana katika dunia nzima hakuna jina lingine lolote watu walilopewa lenye uwezo wa kuwaokoa.”


Ndiyo kusema, Mungu ndiye aliyekuwa akipatanisha watu wote na yeye mwenyewe kwa njia ya Kristo bila kuhesabu makosa yao. Yeye ametupatia ujumbe wa upatanisho.


Katika kuungana pamoja na Kristo, ninyi vilevile munaunganishwa pamoja na wengine wote kuwa makao ya Mungu kwa njia ya Roho wake.


Yeye ni utukufu wenu. Yeye ni Mungu wenu ambaye amewatendea haya mambo makubwa na ya kutisha muliyoona kwa macho yenu wenyewe.


na kila mutu akubali kwamba Yesu ni Bwana, naye Mungu Baba atatukuzwa kwa njia hiyo.


Ninaweza vyote kwa njia ya Kristo anayenitia nguvu.


Kwa maana ukamilifu wote wa Mungu uko ndani ya Kristo katika mwili wake.


Waliimba wimbo wa Musa, mutumishi wa Mungu, na wimbo wa Mwana- Kondoo wakisema: “Ewe Bwana wetu, Mungu Mwenye Uwezo, matendo yako ni makubwa na ya ajabu! Ewe Mufalme wa mataifa, kazi zako ni za haki na za kweli!


Kisha mambo hayo, nikasikia kelele kutoka mbinguni linalosikilika kama vile sauti kubwa ya kundi kubwa la watu ikisema: “Mungu asifiwe! Wokovu, utukufu na uwezo ni vya Mungu wetu. Yeye anastahili utukufu na uwezo.


Mafuriko ya muto Kisoni yaliwapeleka mbali, mafuriko makali ya muto Kisoni. Songa mbele kwa nguvu, ee nafsi yangu!


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ