Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Kutoka 14:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Halafu mimi nitafanya moyo wa mufalme wa Misri kuwa mugumu, naye atawafuatilia. Nami nitajipatia utukufu kwa kumwangamiza yeye na jeshi lake. Halafu Wamisri watatambua kwamba mimi ni Yawe.” Basi, Waisraeli wakafanya hivyo.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Kutoka 14:4
36 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Ulifanya miujiza na maajabu mbele ya Mufalme wa Misri, watumishi wake wote na watu wote wa inchi yake; maana ulijua kwamba waliwagandamiza babu zetu. Ukajipatia utukufu unaokuwa mpaka leo.


na ninyi mupate kuwaelezea watoto wenu na wajukuu wenu jinsi nilivyowachekelea Wamisri kwa kuonyesha vitambulisho vile kati yao. Hivyo mutatambua kwamba mimi ni Yawe.”


Lakini Yawe akaufanya moyo wa mufalme wa Misri kuwa mugumu, akakataa kuwaachilia Waisraeli waondoke.


Kisha Waisraeli wakaenda, wakafanya kama vile walivyoambiwa na Musa na Haruni kulingana na amri ya Yawe.


Wamisri wakawafuata kwa kupitia inchi kavu iliyokuwa katikati ya bahari pamoja na farasi wao, magari yao ya vita na wapanda-farasi wao wote.


Alikwamisha magurudumu ya magari yao, yakakuwa yakienda kwa shida sana. Halafu Wamisri wakasema: “Tuwakimbie Waisraeli! Yawe anawapigania Waisraeli mbele yetu.”


Maana, mufalme wa Misri atafikiri: ‘Hao Waisraeli wanatangatanga, nalo jangwa limewazuia wasiweze kutoka.’


Mufalme wa Misri aliposikia kwamba Waisraeli wamekimbia, yeye na wakubwa wake walibadilisha mafikiri yao, wakasema: “Tumefanya nini kwa kuwaachilia Waisraeli waende zao wasitutumikie tena?”


Yawe akafanya moyo wa mufalme wa Misri kuwa mugumu, naye akawafuatilia Waisraeli ambao walikuwa wameondoka Misri katika uhuru.


Sasa ninajua kwamba Yawe ni mukubwa kuliko miungu yote, maana amewakomboa watu hawa toka katika mikono ya Wamisri ambao waliwatendea ubaya.”


Nitawafanya kuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wenu. Ninyi mutatambua kwamba mimi ni Yawe, Mungu wenu, niliyewatoa katika nira za Wamisri.


Basi, Yawe anasema kwamba sasa utamutambua yeye ni nani. Nitayapiga maji ya muto Nili kwa fimbo hii na maji yote yatageuka kuwa damu.


Lakini nitafanya moyo wa mufalme kuwa mugumu. Na hata kama nitazidisha vitambulisho na maajabu yangu katika inchi ya Misri,


wakati nitakaponyoosha mukono wangu juu ya inchi ya Misri na kuwatoa Waisraeli kati yao. Halafu Wamisri watatambua kwamba mimi ni Yawe.”


Lakini nimewaacha muishi kwa kuonyesha uwezo wangu. Kwa hiyo dunia yote itatambua kwamba mimi ni nani.


Lakini nilijizuiza kufanya hivyo kwa heshima ya jina langu kusudi lisizarauliwe kati ya watu wa mataifa wanaoishi nao, hao walioona nikijijulisha kwa Waisraeli wakati wa kuwatoa katika inchi ya Misri.


Sema hivi: Bwana wetu Yawe anasema hivi: Mimi nitapingana nawe Sidona, na kuonyesha utukufu wangu kati yako. Nitakapotimiza hukumu zangu juu yako na kukuonyesha utakatifu wangu, halafu utatambua kwamba mimi ni Yawe.


Nitakapoifanya inchi ya Misri kuwa jangwa na mali yake yote kunyanganywa, nitakapowaua wakaaji wake wote, halafu watatambua kwamba mimi ni Yawe.


Utawashambulia Waisraeli, kama vile wingu linalotanda juu ya inchi. Wakati huo nitakutuma uishambulie inchi yangu, kusudi mataifa yajue kwamba nimekutumia wewe Gogi kusudi nionyeshe utakatifu wangu mbele yao.


Ndivyo nitakavyofanya kusudi yote yaone ukubwa wangu na utakatifu wangu. Halafu watatambua kwamba mimi ni Yawe.


Watu wote katika inchi watashugulika na kuwazika. Na hilo litakuwa jambo la kuwapatia sifa, siku ile nitakapoonyesha utukufu wangu. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.–


Kwa hiyo, Musa akamwambia Haruni: Kwa tukio hili Yawe amekuonyesha maana ya kile alichosema: Nitajionyesha kuwa mutakatifu kati ya wale wanaokuwa karibu nami, nitatukuzwa mbele ya watu wote! Haruni akanyamaza kimya.


kama vile ilivyoandikwa katika Maandiko Matakatifu: “Mungu ameifanya mioyo yao kuwa migumu, macho yao yasipate kuona na masikio yao yasipate kusikia, na ni hivi wanavyokuwa hata leo.”


Mungu anamwambia mufalme wa Misri katika Maandiko Matakatifu: “Nimekusimika kuwa mufalme kwa sababu hii moja, ni kusudi kwa njia yako nipate kuonyesha uwezo wangu na kusudi jina langu lipate kutangazwa katika dunia yote.”


Basi ni kusema kwamba Mungu anamuhurumia yule anayetaka, na kumufanya mugumu yule anayetaka.


Ilikuwa ni mapenzi ya Yawe mwenyewe kuifanya mioyo ya watu wa mataifa hayo kuwa migumu kusudi wapigane. Alikusudia wasihurumiwe lakini wateketezwe. Ndivyo Yawe alivyomwamuru Musa.


Mimi nitamuchochea Sisera, jemadari wa waaskari wa mufalme Asikie, akuje na waaskari na magari yake kupigana nawe kwenye muto Kisoni, na kumutia katika mikono yako.’ ”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ