Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Kutoka 13:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Na mambo haya yatakuwa ukumbusho, kama vile kitambulisho katika mikono yenu au katika paji la nyuso zenu; kusudi kiwakumbushe siku zote sheria ya Yawe. Maana, Yawe amewatoa katika inchi ya Misri kwa mukono wenye nguvu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Kutoka 13:9
38 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Watu wa Israeli ni watumishi wako na watu wako uliwakomboa kwa uwezo wako na mukono wako wenye nguvu.


Akawaondoa watu wa Israeli kutoka huko. Wema wake unadumu milele.


Akawaondoa kwa mukono wake wenye nguvu na mamlaka. Wema wake unadumu milele.


Wewe uliumba kaskazini na kusini; milima Tabori na Hermoni inakushangilia.


Vizazi hata vizazi mutakumbuka tukio hilo kwa sikukuu kubwa kwa heshima yangu mimi Yawe. Hilo litakuwa agizo la milele kwenu.”


Katika siku ya mwisho ya mwaka wa mia ine na makumi tatu, siku ileile ndipo makabila yote ya Yawe yaliondoka katika inchi ya Misri.


Kama kisha mwana wako akiuliza maana ya jambo hili, utamwambia: ‘Kwa nguvu ya mukono wake, Yawe alitutoa katika inchi ya Misri ambako tulikuwa watumwa.


Jambo hili litakuwa kama kitambulisho katika mukono wako au utepe katika paji la uso wako, kwamba Yawe alitutoa katika inchi ya Misri kwa mukono wenye nguvu.”


Musa akawaambia watu: “Mukumbuke siku hii muliyotoka inchi ya Misri ambako mulikuwa watumwa. Hii ndiyo siku Yawe alipowatoa humo kwa mukono wake wenye nguvu. Katika siku hii, musikule mukate uliotiwa chachu.


Kwa hiyo nitaunyoosha mukono wangu na kupiga inchi ya Misri kwa maajabu ambayo nitayafanya kule. Kisha mufalme atawaacha muondoke.


Mufalme wa Misri hatakusikiliza. Na hapo nitanyoosha mukono wangu wenye nguvu na kuazibu vikali inchi ya Misri na kuwatoa watu wangu, makabila ya Israeli, kutoka Misri. Nitafanya hivyo kwa matendo makubwa ya hukumu juu ya Misri,


hayo yatakupamba kilemba cha neema juu ya kichwa chako, kama mukufu katika shingo yako.


Mwana wangu, shika hekima safi na akili; usiviache vitoweke mbele ya macho yako,


Hakutambua kwamba maisha yake yako katika hatari, mpaka alipojikuta amekuwa kama amechomwa mushale ndani ya moyo, amekuwa kama ndege aliyerukia ndani ya wavu.


Unipige kama muhuri ndani ya moyo wako, kama muhuri katika mikono yako. Maana mapendo yana nguvu kama kifo, nao wivu ni mukali kama kaburi. Kuwaka kwake ni kama kuwaka kwa moto, unawaka kama ulimi wa moto.


Siku hiyo, Yawe atakamata upanga wake mukubwa, mukali na imara, na kuiazibu Leviatani, ile nyoka inayoruka na kuzongazonga. Yawe ataua nyoka mukubwa anayeishi katika bahari.


Bwana wetu Yawe anakuja na nguvu, kwa mukono wake anatawala. Yeye anakuja na mapato yake, anafika na mushahara wake.


Mumoja atasema: “Mimi ni wa Yawe”, mwingine atajiita kwa jina la Yakobo, mwingine ataandika juu ya mukono wake: “Wa Yawe”, na kujitambulisha kwa jina la Israeli.


Nimekuchora wewe katika vitanga vya mikono yangu; kuta zako ninaziona mbele yangu siku zote.


Amuka! Amuka na nguvu, ee mukono wa Yawe! Amuka kama ulivyofanya hapo zamani, nyakati za vizazi vilivyopita. Si wewe ndiwe uliyemukatakata yule nyama mukubwa Rahabu, ukamutoboa yule nyoka mukubwa wa kuogopesha?


Yawe anasema: Mimi ninafanya nanyi agano hili: Roho wangu anayekuwa juu yenu, maneno niliyoyaweka katika kinywa chenu, hayataondoka kwenu hata kidogo, wala kwa watoto na wajukuu wenu, tangu sasa na hata milele.


Yawe anasema hivi: Kama vile ninavyoishi, hata kama wewe Konia mwana wa Yoyakimu, mufalme wa Yuda, ungekuwa wa lazima kwangu kama vile pete yangu ya muhuri ninayovaa kwa mukono wangu wa kuume, ningekuvua.


Na sasa ee Bwana, Mungu wetu, uliyewaondoa watu wako katika inchi ya Misri kwa nguvu yako kubwa na kulifanya jina lako litukuzwe mpaka sasa, tunasema kwamba tumetenda zambi; tumefanya maovu.


Yawe anaamuru kundi lake kwa sauti; waaskari wake ni wengi sana, wanaomutii hawahesabiki. Siku ya Yawe kweli ni kubwa na ya kutisha sana! Nani atakayeweza kuivumilia?


Vishada hivyo vitakuwa ukumbusho kwenu. Kila mara mutakapoviona, mutakumbuka amri zangu zote na kuzifuata, kusudi musifuate mapenzi yenu na yale munayoona kwa macho yenu wenyewe.


Wanafanya matendo yao yote tu kusudi wajionyeshe mbele ya watu. Wanajifungia kwa paji za nyuso vibweta vipana vyenye vikaratasi vya Maandiko Matakatifu. Nao wanavaa kanzu zenye pembe ndefu.


Lakini inasemwa namna gani? “Neno la Mungu liko karibu nawe, liko ndani ya kinywa chako na ndani ya moyo wako.” Neno hili ni ujumbe tunaouhubiri juu ya imani.


Sivyo, lakini neno hili liko karibu nanyi, ndani ya vinywa vyenu na ndani ya mioyo yenu, mupate kulitimiza.


Usisahau kwamba wewe ulikuwa mutumwa katika inchi ya Misri, nami Yawe, Mungu wako, nikakutoa huko kwa mukono wenye nguvu na mukono ulionyooshwa. Ndiyo maana mimi Yawe, Mungu wako, nimekuamuru kushika siku ya Sabato.


Ninyi mutawajibu hivi: ‘Sisi tulikuwa watumwa wa mufalme wa Misri, na Yawe akatuokoa kwa mukono wake wenye nguvu.


Muweke ndani ya moyo wenu maneno hayo ninayowaamuru leo


Muyafunge katika mikono yenu na kuyavaa katika paji za nyuso zenu kama vile ukumbusho.


Kwa sababu hiyo, kwa muda wa siku moja tu utapatwa na mapigo ya mauti, huzuni na njaa. Na zaidi ya hiyo utateketezwa kwa moto, kwa maana Bwana wetu, Mungu anayeuhukumu, ni mwenye uwezo.”


Walimwacha Yawe, Mungu wa wazee wao, ambaye aliwaondoa katika inchi ya Misri, wakaifuata miungu mingine, miungu iliyoabudiwa na watu walioishi kandokando yao. Waliinama mbele ya miungu hiyo, wakamukasirikisha sana Yawe.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ