Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Kutoka 13:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Musa akawaambia watu: “Mukumbuke siku hii muliyotoka inchi ya Misri ambako mulikuwa watumwa. Hii ndiyo siku Yawe alipowatoa humo kwa mukono wake wenye nguvu. Katika siku hii, musikule mukate uliotiwa chachu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Kutoka 13:3
58 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wazao wako watarudi hapa katika kizazi cha ine, kwa sababu uovu wa Waamori haujakamilika bado.”


maana watu wa mataifa mengine watasikia sifa zako na juu ya nguvu na uwezo wako, mutu yule akikuja na kuomba akielekea nyumba hii,


Mukumbuke matendo ya ajabu aliyotenda, maajabu yake na hukumu alizotoa,


Watu wa Israeli ni watumishi wako na watu wako uliwakomboa kwa uwezo wako na mukono wako wenye nguvu.


Ulifanya miujiza na maajabu mbele ya Mufalme wa Misri, watumishi wake wote na watu wote wa inchi yake; maana ulijua kwamba waliwagandamiza babu zetu. Ukajipatia utukufu unaokuwa mpaka leo.


Mukumbuke matendo ya ajabu aliyotenda, miujiza yake na hukumu alizotoa,


Watu wa Israeli walipotoka Misri, wazao wa Yakobo walipotoka katika inchi ya kigeni,


Akawaondoa watu wa Israeli kutoka huko. Wema wake unadumu milele.


Akawaondoa kwa mukono wake wenye nguvu na mamlaka. Wema wake unadumu milele.


Mukono wako unajaa nguvu, mukono wako una nguvu na umeshinda!


Yawe akaendelea kusema: “Kwa muda wa siku saba, mutakula mikate isiyotiwa chachu. Siku ya kwanza ya siku hizo saba, mutaondoa chachu katika nyumba zenu. Mutu yeyote akikula kitu kilichotiwa chachu katika muda ule wa siku saba, anapaswa kuondolewa kati ya Waisraeli.


Mutashika sikukuu hii ya Mikate Isiyotiwa Chachu kama ukumbusho wa siku nilipowatoa ninyi vikundi vya Israeli kutoka Misri. Sikukuu hiyo itashikwa na vizazi vyenu vyote vinavyokuja, kama agizo la milele.


Katika siku hizo saba, musikuwe na chachu yoyote katika nyumba zenu. Mutu yeyote, akuwe mugeni au mwenyeji, akikula kitu kilichotiwa chachu, ataondolewa katika kusanyiko la Waisraeli.


“Mwezi huu utakuwa kwenu mwezi wa kwanza wa mwaka.


Katika siku ya mwisho ya mwaka wa mia ine na makumi tatu, siku ileile ndipo makabila yote ya Yawe yaliondoka katika inchi ya Misri.


Usiku ule ambao Yawe alikesha kwa kuwatoa Waisraeli katika inchi ya Misri, unapaswa kukumbukwa na Waisraeli wote na vizazi vyao vyote, kama usiku wa kukesha kwa heshima ya Yawe.


Watakula nyama hiyo usiku uleule kisha kuichoma. Wataikula pamoja na mukate usiotiwa chachu na mboga chungu za majani.


Kama kisha mwana wako akiuliza maana ya jambo hili, utamwambia: ‘Kwa nguvu ya mukono wake, Yawe alitutoa katika inchi ya Misri ambako tulikuwa watumwa.


Na mambo haya yatakuwa ukumbusho, kama vile kitambulisho katika mikono yenu au katika paji la nyuso zenu; kusudi kiwakumbushe siku zote sheria ya Yawe. Maana, Yawe amewatoa katika inchi ya Misri kwa mukono wenye nguvu.


Mimi ni Yawe, Mungu wako, niliyekutoa katika inchi ya Misri, ambako ulikuwa mutumwa.


Mutafanya sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu kama vile nilivyowaagiza. Mutakula mikate isiyotiwa chachu kwa siku saba wakati uliopangwa katika mwezi wa Abibu, kwa sababu katika mwezi ule mulitoka Misri. Mutu yeyote asikuje mbele yangu mikono mitupu.


Kwa hiyo nitaunyoosha mukono wangu na kupiga inchi ya Misri kwa maajabu ambayo nitayafanya kule. Kisha mufalme atawaacha muondoke.


Mutashika sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu. Kwa muda wa siku saba mutakula mikate isiyotiwa chachu wakati uliopangwa katika mwezi wa Abibu, kama vile nilivyowaamuru, kwa sababu katika mwezi huo wa Abibu mulitoka Misri.


Lakini Yawe akamujibu Musa: “Sasa utaona jinsi nitakavyomutendea mufalme wa Misri. Kwa nguvu atalazimishwa kuwaacha watu wangu watoke. Kwa nguvu atawafukuza waondoke katika inchi yake.”


Kwa hiyo, uwaambie Waisraeli hivi: ‘Mimi ni Yawe! Mimi nitawatoa katika nira mulizowekewa na Wamisri. Nitawaokoa toka utumwa wenu. Nitanyoosha mukono wangu wenye nguvu na kuwaazibu vikali Wamisri na kuwakomboa ninyi.


Nitawafanya kuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wenu. Ninyi mutatambua kwamba mimi ni Yawe, Mungu wenu, niliyewatoa katika nira za Wamisri.


Mufalme wa Misri hatakusikiliza. Na hapo nitanyoosha mukono wangu wenye nguvu na kuazibu vikali inchi ya Misri na kuwatoa watu wangu, makabila ya Israeli, kutoka Misri. Nitafanya hivyo kwa matendo makubwa ya hukumu juu ya Misri,


Yawe, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Nilifanya agano na babu zenu nilipowatoa toka inchi ya Misri ambako walikuwa watumwa, nikawaambia:


Na sasa ee Bwana, Mungu wetu, uliyewaondoa watu wako katika inchi ya Misri kwa nguvu yako kubwa na kulifanya jina lako litukuzwe mpaka sasa, tunasema kwamba tumetenda zambi; tumefanya maovu.


Mutakapoingia ndani ya nyumba, muwasalimie watu wanaokuwa mule, mukisema: ‘Amani kwenu.’


Halafu akatwaa mukate, akaubariki, kisha akaumega na kuwapa akisema: “Huu ni mwili wangu [unaotolewa kwa ajili yenu. Mufanye hivi kwa kunikumbuka.”


na alipokwisha kumushukuru Mungu, akaumega akisema: “Huu ni mwili wangu unaotolewa kwa ajili yenu. Mufanye hivi kwa kunikumbuka.”


Kwa hiyo tufanye karamu yetu ya Pasaka pasipo kutumia mikate iliyotiwa chachu; ni kusema pasipo zambi na uovu. Lakini tutumie mikate isiyotiwa chachu; ni kusema katika usafi na ukweli.


na kutambua jinsi uwezo wake unavyokuwa mukubwa sana kwa ajili yetu sisi waamini, akizitumia nguvu zake kubwa sana.


lakini utamwua. Mukono wako unapaswa ukuwe wa kwanza wakati wa kumwua halafu wengine wote watafuata vilevile.


Umupige mawe mpaka akufe, kwa sababu amejaribu kukuvuta mbali kutoka kwa Yawe, Mungu wako, ambaye alikutoa toka utumwa katika inchi ya Misri.


Mufuate na kumwogopa Yawe, Mungu wenu, na kushika amri zake na kutii sauti yake. Mumutumikie na kuambatana naye.


Lakini nabii huyo au mutabiri wa kutumia ndoto atauawa, kwa sababu atakuwa amewafundisha uasi mbele ya Yawe, Mungu wenu, aliyewatoa katika inchi ya Misri na kuwakomboa kutoka katika utumwa, kusudi muache njia ambayo Yawe, Mungu wenu, aliwaamuru kufuata. Hivi ndivyo mutakavyokomesha uovu kati yenu.


Mukumbuke kwamba ninyi mulikuwa watumwa huko Misri na Yawe, Mungu wenu, aliwakomboa; ndiyo maana leo ninawaamuru hivyo.


“Mushike mwezi wa Abibu na kufanya Pasaka kwa heshima ya Yawe, Mungu wenu. Maana katika mwezi huo wa Abibu, Yawe, Mungu wenu aliwatoa Misri wakati wa usiku.


Mukumbuke kwamba mulikuwa watumwa kule Misri na mukuwe waangalifu kufuata masharti haya.


Musikule sadaka hiyo na mikate iliyotiwa chachu. Kwa muda wa siku saba mutakula mikate isiyotiwa chachu, nayo ni mikate ya mateso – kwa sababu mulitoka Misri kwa haraka; kwa hiyo, muda wote mutakaoishi mutakumbuka ile siku mulipotoka Misri.


Mukumbuke kwamba ninyi mulikuwa watumwa katika inchi ya Misri, na Yawe, Mungu wenu, akawakomboa kutoka huko. Kwa hiyo ninawapa amri hiyo.


Mutakumbuka kwamba ninyi mulikuwa watumwa katika inchi ya Misri; kwa hiyo ninawapa ninyi amri hii.


Basi, Yawe akatutoa huko Misri kwa mukono wake wa nguvu ulionyooshwa, kwa vitisho, vitambulisho na maajabu.


Kuna Mungu yeyote mwingine aliyejaribu hata kidogo kwenda kujitwalia taifa lake kutoka taifa lingine, kama vile Yawe, Mungu wenu, alivyofanya, kwa kutumia majaribio, vitambulisho, maajabu, vita, na vitisho? Hapana. Lakini mulishuhudia kwa macho yenu namna Yawe alivyofanya kwa mukono wake wenye nguvu kabisa kule Misri.


Usisahau kwamba wewe ulikuwa mutumwa katika inchi ya Misri, nami Yawe, Mungu wako, nikakutoa huko kwa mukono wenye nguvu na mukono ulionyooshwa. Ndiyo maana mimi Yawe, Mungu wako, nimekuamuru kushika siku ya Sabato.


“Mimi ni Yawe, Mungu wako, niliyekutoa katika inchi ya Misri, ambako ulikuwa mutumwa.


muhakikishe kwamba hamutamusahau Yawe aliyewatoa Misri ambako mulikuwa watumwa.


Ninyi mutawajibu hivi: ‘Sisi tulikuwa watumwa wa mufalme wa Misri, na Yawe akatuokoa kwa mukono wake wenye nguvu.


Lakini ni kwa sababu Yawe anawapenda na anashika kiapo alichowaapia babu zenu, ndiyo maana aliwaokoa kwa nguvu zake kubwa na kuwaokoa toka katika utumwa, toka mikono ya mufalme wa Misri.


musikuwe na kiburi na kumusahau Yawe, Mungu wenu, aliyewatoa katika inchi ya Misri, pahali mulipokuwa watumwa.


“Basi, Yawe akaniambia: ‘Ondoka, ushuke chini ya mulima upesi, kwa sababu watu wako uliowatoa Misri wamepotoka. Wameacha upesi njia niliyowaamuru wafuate na wamejifanyia sanamu ya kuyeyushwa’.


Maana, Yawe, Mungu wetu, ndiye aliyetutoa sisi pamoja na wazee wetu katika inchi ya Misri tulikokuwa watumwa, tukayaona kwa macho yetu wenyewe matendo ya ajabu aliyotenda. Akatulinda katika safari zetu zote na kati ya watu wote ambao tulipita kati yao.


Walimwacha Yawe, Mungu wa wazee wao, ambaye aliwaondoa katika inchi ya Misri, wakaifuata miungu mingine, miungu iliyoabudiwa na watu walioishi kandokando yao. Waliinama mbele ya miungu hiyo, wakamukasirikisha sana Yawe.


Yawe akawapelekea nabii, naye akawaambia: “Yawe, Mungu wa Israeli, anasema hivi: ‘Niliwaondoa katika inchi ya Misri ambako mulikuwa watumwa,


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ