Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Kutoka 13:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 “Unitakasie wazaliwa wote wa kwanza, maana wazaliwa wote wa kwanza wa Waisraeli ni wangu, ikuwe wanaume au wanyama.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Kutoka 13:2
19 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Tunaahidi kuleta kila mwaka malimbuko yetu ya mazao na ya matunda ya kila muti kwenye nyumba ya Yawe.


Kwa kufuata vile ilivyoandikwa katika Sheria kila muzaliwa wa kwanza wa kiume kati ya wana wetu, katika nyumba zetu, atapelekwa katika nyumba ya Mungu wetu kwa makuhani wanaotumika mule, vilevile tutapeleka kila muzaliwa wa kwanza dume wa ngombe zetu, mbuzi zetu na kondoo zetu.


Usikawie kunitolea sehemu yangu kutokana na wingi wa mazao yako na divai yako. Mutanipa wazaliwa wenu wa kwanza wanaume.


Mazao ya kwanza ya shamba lako utayaleta katika nyumba yangu mimi Yawe, Mungu wako. Usipike mwana-kondoo au mwana-mbuzi katika maziwa ya mama yake.


Nawe utamwambia mufalme wa Misri kwamba Yawe anasema hivi: ‘Israeli ni mwana wangu, muzaliwa wangu wa kwanza.


Tena, wana wako na wabinti zako ulionizalia uliwatwaa, ukawatambikia kwa sanamu zako wapate kukuliwa. Unazani uzinzi wako ulikuwa ni jambo dogo?


Jambo hili la kuwachinja watoto wangu kwa kuwa sadaka ya kuteketeza kwa ajili ya sanamu zako ni jambo dogo?


Hairuhusiwi kumutakasa muzaliwa wa kwanza wa nyama. Kufuatana na sheria, huyo ni wa Yawe, akuwe ni ngombe au kondoo.


Kila muzaliwa wa kwanza ambaye Waisraeli watanitolea, akiwa muzaliwa wa kwanza wa wanadamu, au wa nyama, atakuwa wako. Lakini unaweza kuwakomboa wazaliwa wa kwanza wote wa wanadamu, na kila muzaliwa wa kwanza wa nyama anayekuwa muchafu.


Sasa nimechagua Walawi kati ya Waisraeli wote, pahali pa kila muzaliwa wa kwanza mwanaume anayefungua tumbo la mama yake katika kila jamaa ya Israeli. Walawi ni wangu,


maana kila muzaliwa wa kwanza katika Israeli ni wangu. Wakati nilipowaua wazaliwa wa kwanza wote wa Wamisri nilijitakasia kila muzaliwa wa kwanza katika Israeli; kila muzaliwa wa kwanza wa mwanadamu hata wa nyama; wao watakuwa wangu. Mimi ni Yawe.


Imeandikwa katika Sheria ya Bwana: “Kila muzaliwa wa kwanza wa kiume atatolewa kwa Bwana.”


“Umutolee Yawe, Mungu wako, wazaliwa wote wa kwanza dume wa kundi lako la ngombe na kondoo. Usiwafanyizishe ngombe hao kazi na kondoo hao usiwakate manyoya.


Lakini ninyi mumefikia kwenye mukutano wa furaha wa wazaliwa wa kwanza wa Mungu walioandikwa majina zao katika mbingu. Mumefikia vilevile karibu na Mungu, anayekuwa mwamuzi wa watu wote na kwenye nafsi kunapokuwa roho za watu wenye haki waliofanywa kuwa wakamilifu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ