Basi, ile damu itakuwa kitambulisho chenu cha kuonyesha nyumba mutakamokuwa. Nami nitakapoiona ile damu, nitawapita ninyi, hamutapatwa na hasara yoyote wakati nitakapoipiga inchi ya Misri.
akamwambia hivi: Pita katikati ya Yerusalema, upate kutia kitambulisho kwenye vipaji vya nyuso za watu wanaohuzunika na kulia kwa sababu ya machukizo yote yanayotendeka katika muji huu.
Basi munazania itakuwa namna gani? Hataazibiwa vikali zaidi yule anayemuzarau Mwana wa Mungu na kuihesabu kuwa bure damu ya agano la Mungu iliyomutakasa na kumutukana Roho wa neema?
Kwa njia ya imani, alianzisha sikukuu ya Pasaka, na kuamuru damu inyunyizwe, kusudi malaika mwangamizaji asiwaue wazaliwa wa kwanza wanaume wa Waisraeli.
Mungu Baba aliwachagua ninyi tangu mbele kufuatana na mupango wake na kufanywa watakatifu na Roho, mupate kumutii Yesu Kristo na kusafishwa kwa damu yake. Ninawatakia neema na amani kwa uwingi.