Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Kutoka 12:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Muwaambie Waisraeli wote pamoja kwamba katika siku ya kumi ya mwezi huu, mutatwaa mwana-kondoo mumoja kwa kila jamaa moja.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Kutoka 12:3
26 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Abrahamu akamujibu: “Mwana wangu, Mungu mwenyewe atatujalia mwana-kondoo wa sadaka ya kuteketezwa.” Basi, wakaendelea na safari yao.


naye Abeli akamutolea Mungu sadaka ya wazao wa kwanza wa kondoo wake na nyama nono. Yawe akapendezwa na Abeli pamoja na sadaka yake,


Kisha Yosia akawapa watu, wana-mbuzi yapata elfu makumi tatu, na ngombe dume elfu tatu, wote hawa toka katika makundi ya mufalme.


“Mwezi huu utakuwa kwenu mwezi wa kwanza wa mwaka.


Basi, Musa akawaita wazee wote wa Waisraeli, akawaambia: “Muchague kila mumoja wenu, kulingana na jamaa yake, mwana-kondoo na kumuchinja kwa sikukuu ya Pasaka.


Kama jamaa moja ni ndogo sana hata isiweze kumaliza kondoo mumoja, itashirikiana na jamaa jirani kadiri ya hesabu ya watu wake. Kisha watachagua nyama ambaye kila mutu ataweza kula.


Mutamuweka nyama yule mpaka siku ya kumi na ine ya mwezi huu. Siku hiyo, Waisraeli watawachinja nyama wale wakati wa magaribi.


Yawe akamwambia Musa: “Kwa nini munanililia? Uwaambie Waisraeli waendelee mbele.


wakamwambia Musa: Sema nasi wewe mwenyewe, nasi tutakusikiliza. Lakini Yawe asiseme nasi, tusikufe.


Haruni akawaambia maneno yote Yawe aliyokuwa amemwagiza Musa na kufanya vile vitambulisho mbele ya watu wote.


Kwa hiyo, uwaambie Waisraeli hivi: ‘Mimi ni Yawe! Mimi nitawatoa katika nira mulizowekewa na Wamisri. Nitawaokoa toka utumwa wenu. Nitanyoosha mukono wangu wenye nguvu na kuwaazibu vikali Wamisri na kuwakomboa ninyi.


Katika mwaka wa makumi mbili na tano tangu tulipopelekwa katika uhamisho, siku ya kumi ya mwezi wa kwanza, siku hiyo Yawe alinijaza uwezo wake. Ilikuwa mwaka wa kumi na ine tangu pale Yerusalema ulipotekwa.


Uwaambie Waisraeli kwamba kama mutu anapenda kumutolea Yawe sadaka ya nyama, nyama huyo atamuchagua kutoka kundi lake la ngombe, kondoo au mbuzi.


na kumuletea Yawe sadaka yake kwa ajili ya kosa. Kwa ajili ya zambi aliyotenda ataleta kondoo dike au mbuzi dike kutoka kundi lake amutoe sadaka kwa ajili ya zambi. Naye kuhani atamufanyia ibada ya upatanisho kwa ajili ya zambi yake.


Hivi ndivyo vitu vitakavyotolewa pamoja na kila mwana-ngombe dume, kondoo dume au mbuzi.


Kesho yake Yoane akamwona Yesu akikuja kwake, akasema: “Angalia Mwana-Kondoo wa Mungu anayeondoa zambi ya dunia!


Wakati alipomwona Yesu akipita, akasema: “Angalia Mwana-Kondoo wa Mungu.”


Siku sita mbele ya Pasaka, Yesu alifika Betania, kwao Lazaro, yule mutu Yesu aliyemufufua.


Kesho yake lile kundi kubwa la watu waliofika kwa sikukuu ya Pasaka wakasikia kwamba Yesu alikuwa katika njia kuja Yerusalema.


Basi mujitakase, mukiondoa ile chachu ya zamani ya zambi. Hivi mutakuwa kama donge jipya, lisilotiwa chachu, sawa vile munavyokuwa kwa kweli. Mufanye vile kwa maana Kristo amekwisha kutolewa sadaka kwa ajili yetu kama vile kondoo wa Pasaka.


Kwa hiyo kesho asubui wote mutakuja mbele yangu, kabila kwa kabila. Kabila nitakalolichagua litakwenda mbele, ukoo kwa ukoo. Ukoo nitakaouchagua utakwenda mbele, jamaa kwa jamaa. Na jamaa nitakayoichagua itakwenda mbele, mutu mumoja mumoja.


Wakaaji wote wa dunia watamwabudu, ndio wale wote ambao tangia kuumbwa kwa dunia, majina yao hayakuandikwa katika kitabu cha uzima cha Mwana-Kondoo aliyechinjwa.


Kwa hiyo Samweli alitwaa mwana-kondoo anayenyonya akamutolea Yawe kama sadaka ya kuteketezwa. Kisha Samweli akamulilia Yawe kwa ajili ya Waisraeli, naye akajibu kilio chake.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ