Katika mwaka wa kumi na mbili wa utawala wa mufalme Ahasuero, katika mwezi wa kwanza unaoitwa Nisani, wakapiga Purimu, maana yake kura, mbele ya Hamani kusudi ajue mwezi na siku ya kuwaangamiza. Basi kura ikaangukia mwezi wa kumi na mbili unaoitwa Adari.
Basi, mutakula mikate isiyotiwa chachu kuanzia magaribi ya siku ya kumi na ine ya mwezi wa kwanza, mpaka magaribi ya siku ya makumi mbili na moja ya mwezi uleule wa kwanza.
Musa akawaambia watu: “Mukumbuke siku hii muliyotoka inchi ya Misri ambako mulikuwa watumwa. Hii ndiyo siku Yawe alipowatoa humo kwa mukono wake wenye nguvu. Katika siku hii, musikule mukate uliotiwa chachu.
Mutafanya sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu kama vile nilivyowaagiza. Mutakula mikate isiyotiwa chachu kwa siku saba wakati uliopangwa katika mwezi wa Abibu, kwa sababu katika mwezi ule mulitoka Misri. Mutu yeyote asikuje mbele yangu mikono mitupu.
Mutashika sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu. Kwa muda wa siku saba mutakula mikate isiyotiwa chachu wakati uliopangwa katika mwezi wa Abibu, kama vile nilivyowaamuru, kwa sababu katika mwezi huo wa Abibu mulitoka Misri.
“Mushike mwezi wa Abibu na kufanya Pasaka kwa heshima ya Yawe, Mungu wenu. Maana katika mwezi huo wa Abibu, Yawe, Mungu wenu aliwatoa Misri wakati wa usiku.