Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Kutoka 12:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 “Mwezi huu utakuwa kwenu mwezi wa kwanza wa mwaka.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Kutoka 12:2
14 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Katika mwaka wa kumi na mbili wa utawala wa mufalme Ahasuero, katika mwezi wa kwanza unaoitwa Nisani, wakapiga Purimu, maana yake kura, mbele ya Hamani kusudi ajue mwezi na siku ya kuwaangamiza. Basi kura ikaangukia mwezi wa kumi na mbili unaoitwa Adari.


Yawe akamwambia Musa na Haruni, walipokuwa wangali katika inchi ya Misri:


Basi, mutakula mikate isiyotiwa chachu kuanzia magaribi ya siku ya kumi na ine ya mwezi wa kwanza, mpaka magaribi ya siku ya makumi mbili na moja ya mwezi uleule wa kwanza.


Muwaambie Waisraeli wote pamoja kwamba katika siku ya kumi ya mwezi huu, mutatwaa mwana-kondoo mumoja kwa kila jamaa moja.


Musa akawaambia watu: “Mukumbuke siku hii muliyotoka inchi ya Misri ambako mulikuwa watumwa. Hii ndiyo siku Yawe alipowatoa humo kwa mukono wake wenye nguvu. Katika siku hii, musikule mukate uliotiwa chachu.


Siku hii, mwezi wa kwanza wa Abibu, mutaondoka katika inchi ya Misri.


Mutafanya sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu kama vile nilivyowaagiza. Mutakula mikate isiyotiwa chachu kwa siku saba wakati uliopangwa katika mwezi wa Abibu, kwa sababu katika mwezi ule mulitoka Misri. Mutu yeyote asikuje mbele yangu mikono mitupu.


Mutashika sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu. Kwa muda wa siku saba mutakula mikate isiyotiwa chachu wakati uliopangwa katika mwezi wa Abibu, kama vile nilivyowaamuru, kwa sababu katika mwezi huo wa Abibu mulitoka Misri.


Katika siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza mwaka wa pili kisha kutoka Misri, hema takatifu likasimikwa.


Bwana wetu Yawe anasema hivi: Siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza, mutatoa sadaka ya mwana-ngombe dume asiyekuwa na kilema kwa kutakasa hekalu langu.


Siku ya kumi na ine ya mwezi wa kwanza, mutafanya sikukuu ya Pasaka. Kwa muda wa siku saba, mutakula mikate isiyotiwa chachu.


Magaribi ya siku ya kumi na ine ya mwezi wa kwanza mutafanya kwa heshima yangu mimi Yawe sikukuu ya Pasaka.


Siku ya kumi na ine ya mwezi wa kwanza ni Pasaka ya Yawe.


“Mushike mwezi wa Abibu na kufanya Pasaka kwa heshima ya Yawe, Mungu wenu. Maana katika mwezi huo wa Abibu, Yawe, Mungu wenu aliwatoa Misri wakati wa usiku.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ