Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Kutoka 11:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Musa akamalizia kwa kumwambia mufalme: “Watumishi wako hawa watanifikia na kuinama mbele yangu kwa heshima, wakinisihi niondoke katika inchi ya Misri, mimi pamoja na watu wote wanaonifuata. Nyuma ya hayo, nitaondoka.” Kisha Musa, akiwa amekasirika, akaondoka kwa mufalme wa Misri.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Kutoka 11:8
18 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Beni-Hadadi akamutumia Ahabu ujumbe huu: “Miungu iniue ikiwa kule Samaria kutabakia mavumbi ya kutosha kwa kujaza vitanga vya mikono kwa kila mumoja wa watu wangu wengi wanaonifuata!”


Basi, mufalme Yoramu akaondoka pamoja na mufalme wa Yuda na mufalme wa Edomu. Nyuma ya kusafiri kwa muda wa siku saba, maji yakawaishia. Hawakukuwa na maji kwa ajili ya waaskari wao wala kwa nyama wao.


Niliposikia malalamiko yao, nikakasirika sana.


Kutoka Mukubwa wa waimbaji: kwa vyombo vyenye nyuzi nane. Zaburi ya Daudi.


Musa naye akamwambia: “Sawa! Kama vile ulivyosema sitakuja kukuona tena.”


Wafalme watakushugulikia, na malkia watakutengenezea chakula. Watainama mbele yako uso mpaka chini, na kulambula mavumbi ya miguu yako. Halafu utatambua kwamba mimi ni Yawe; wote wanaonitegemea hawatapata haya.


Nitawasukuma watesaji wako wakule miili yao wenyewe; watalewa damu yao wenyewe kama divai. Halafu wanadamu wote watatambua kwamba mimi ni Yawe, Mwokozi wako, Mukombozi wako, Mwenye Nguvu wa Yakobo.


Basi, Roho akaninyanyua juu na kunipeleka mbali. Yawe alinijaza uwezo wake. Nami nikaenda nikiwa na uchungu na hasira katika roho yangu.


Kwa hiyo, mufalme Nebukadneza akawaka hasira, sura yake ikabadilika kwa chuki juu ya Sadiraki, Mesaki na Abedenego. Akaamuru kwamba moto wa furu uongezwe mara saba kuliko kawaida yake.


(Musa alikuwa mutu munyenyekevu kuliko watu wengine wote waliokuwa katika dunia.)


Yesu akawakazia macho kwa kasirani, akihuzunika kwa sababu ya ugumu wao. Akamwambia yule mutu: “Nyoosha mukono wako.” Akaunyoosha, nao ukakuwa muzima tena.


Na jibu hili litatolewa: ‘Ni kwa sababu walivunja agano la Yawe, Mungu wa wazee wao ambalo alifanya nao alipowatoa katika inchi ya Misri.


Watakonda kwa njaa, wataangamizwa kwa homa kali. Nitaleta nyama wenye meno makali kuwashambulia, na nyoka wenye sumu wanaotambaa juu ya mavumbi.


Kwa njia ya imani, Musa alitoka katika inchi ya Misri bila kuogopa kasirani ya mufalme. Na kama vile mutu mwenye kumwona Mungu asiyeonekana, yeye hakurudi nyuma.


Angalia, nitakupa watu wa kikundi chenye kuabudu Shetani, ndio wale wasema uongo wanaojidai kwamba wao ni Wayuda, lakini ni wadanganyifu. Hakika nitawalazimisha kupiga magoti mbele yako, nao watajua ya kuwa mimi ninakupenda.


Baraka akayaita makabila ya Nafutali na Zebuluni kule Kedesi. Watu elfu kumi wakamufuata. Debora akaenda pamoja naye.


Basi, akawaambia watu wa Sukoti: “Tafazali, muwape wenzangu hawa mikate maana wamechoka sana; nami ninaendelea kuwafuatilia Sadaka na Kivuli, wafalme wa Midiani?”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ