Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Kutoka 11:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Yawe akawafanya Waisraeli wapate kukubaliwa mbele ya Wamisri. Tena, Musa mwenyewe akakuwa mutu mukubwa sana katika inchi ya Misri na mbele ya wakubwa na mufalme na watu wote.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Kutoka 11:3
14 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Nitakufanya wewe kuwa taifa kubwa, nitakubariki na kutukuza jina lako, nawe utakuwa baraka.


Yawe alikuwa pamoja na Yosefu na kumutendea mema, hata kumufanya apate kukubaliwa mbele ya mukubwa wa kifungo.


Tangu wakati ule nimekuwa pamoja nawe kokote ulikokwenda na nimewaangamiza waadui zako wote mbele yako. Nitakufanya kuwa mwenye utukufu kama wakubwa wengine katika dunia.


Mordekayi sasa akakuwa mutu mwenye madaraka makubwa katika nyumba ya kifalme, na habari zake zikaenea katika majimbo yote kwamba uwezo wake ulikuwa unazidi kuongezeka.


Aliwafanya wale waliowaangamiza wawaonee huruma.


Waisraeli walikuwa wamekwisha kufanya kama vile Musa alivyowaagiza pale mbele. Waliwaomba Wamisri wawapatie vyombo vya feza na zahabu na nguo.


Naye Yawe alikwisha kuwafanya Waisraeli wapate kukubaliwa mbele ya Wamisri, nao Wamisri wakawapa kila kitu walichoomba. Ndivyo Waisraeli walivyonyanganya Wamisri mali yao.


“Tena nitafanya Waisraeli wapate kukubaliwa mbele ya Wamisri na mutakapoondoka Misri, hamutatoka mikono mitupu.


Wazao wa wale waliokutesa, watakuja na kuinama uso mpaka chini mbele yako. Wote wale waliokuzarau, watapiga magoti kwenye miguu yako. Watakuita: “Muji wa Yawe”, “Sayuni”, “Muji wa Mutakatifu wa Israeli”.


Musa akafundishwa mambo yote ya hekima ya Wamisri, akakuwa mwenye uwezo sana katika masemi yake na matendo yake.


Hakujatokea tena nabii katika Israeli kama Musa, ambaye Yawe alisema naye uso kwa uso.


Hakuna nabii mwingine ambaye alifanya vitambulisho na miujiza kama ile ambayo Yawe aliyomutuma Musa afanye mbele ya mufalme wa Misri, wakubwa wake na inchi yake yote.


Katika siku hiyo Yawe akamutukuza Yoshua mbele ya Waisraeli wote, nao wakamuheshimu Yoshua maisha yake yote kama walivyomuheshimu Musa katika maisha yake.


Angalia, nitakupa watu wa kikundi chenye kuabudu Shetani, ndio wale wasema uongo wanaojidai kwamba wao ni Wayuda, lakini ni wadanganyifu. Hakika nitawalazimisha kupiga magoti mbele yako, nao watajua ya kuwa mimi ninakupenda.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ