Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Kutoka 11:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Yawe akamwambia Musa: “Kungali bado pigo moja nitakalomuletea mufalme wa Misri na inchi ya Misri. Kisha atawaacha muondoke hapa. Naye atakapowaacha muondoke, atawafukuza kwa lote.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Kutoka 11:1
11 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Hata hivyo, nitaazibu taifa watakalotumikia na kwa mwisho watatoka wakiwa na mali nyingi.


Kila mara uko na ushuhuda juu yangu, unaongeza hasira yako juu yangu, unaniletea waadui wapya wanishambulie.


Katikati ya usiku, Yawe akawaua wazaliwa wa kwanza wote wa Misri. Wote walikufa, tangu muzaliwa wa kwanza wa mufalme wa Misri, murizi wa ufalme, mpaka muzaliwa wa kwanza wa mufungwa katika kifungo. Hata wazaliwa wa kwanza wa nyama nao walikufa.


Kwa hiyo nitaunyoosha mukono wangu na kupiga inchi ya Misri kwa maajabu ambayo nitayafanya kule. Kisha mufalme atawaacha muondoke.


Lakini Yawe akamujibu Musa: “Sasa utaona jinsi nitakavyomutendea mufalme wa Misri. Kwa nguvu atalazimishwa kuwaacha watu wangu watoke. Kwa nguvu atawafukuza waondoke katika inchi yake.”


Maana mara hii, wewe mwenyewe, wakubwa wako na watu wako mutapatwa na mapigo yangu makali. Nawe utatambua kwamba hakuna yeyote katika dunia anayekuwa kama mimi.


Kama mukiendelea kunipinga na kukataa kunisikiliza, nitazidisha tena azabu yenu mara saba kadiri ya wingi wa zambi zenu.


Kuna Mungu yeyote mwingine aliyejaribu hata kidogo kwenda kujitwalia taifa lake kutoka taifa lingine, kama vile Yawe, Mungu wenu, alivyofanya, kwa kutumia majaribio, vitambulisho, maajabu, vita, na vitisho? Hapana. Lakini mulishuhudia kwa macho yenu namna Yawe alivyofanya kwa mukono wake wenye nguvu kabisa kule Misri.


Watu wakaunguzwa na lile joto kali, hata wakatukana jina la Mungu anayekuwa na uwezo wa kuamuru mapigo yale. Wakakataa kugeuka toka zambi zao na kumutukuza Mungu.


Watu wakauliza: “Tutamutolea nini kwa malipo ya makosa?” Wao wakawajibu: “Sanamu tano za zahabu mufano wa majipu, na sanamu tano za zahabu mufano wa panya, kufuatana na hesabu ya wakubwa wa Wafilistini, maana kulikuwa pigo moja tu, kwa ninyi wote na kwa wakubwa wenu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ