Kutoka 10:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
8 Hapo, Musa na Haruni wakaitwa warudi kwa mufalme wa Misri, naye akawaambia: “Muende mumutumikie Yawe, Mungu wenu. Lakini, ninauliza, ni nani watakaokwenda pamoja nanyi?”
Kisha, mufalme wa Misri akamwita Musa, akamwambia: “Mwende mumutumikie Yawe. Watoto wenu vilevile wanaweza kwenda pamoja nanyi. Lakini kondoo na mbuzi, na ngombe wenu wabaki.”
Halafu mufalme wa Misri akaita Musa na Haruni, usiku uleule, akawaambia: “Musimame! Muondoke kati ya watu wangu. Muende, ninyi pamoja na wale Waisraeli, mumutumikie Yawe kama vile mulivyosema.
Musa akamujibu: “Mara tu nitakapokuacha, kesho nitamwomba Yawe makundi haya ya mainzi yatoweke kwako wewe mufalme, wakubwa wako na watu wako. Lakini wewe usitudanganye tena kwa kukataa kuwaacha watu kwenda kutoa sadaka kwa Yawe.”