Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Kutoka 10:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Viongozi wa mufalme wakamwuliza: “Mutu huyu atatusumbua mpaka wakati gani? Uwaache watu hawa wajiendee wamutumikie Yawe, Mungu wao. Haujali kwamba inchi ya Misri inaangamia?”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Kutoka 10:7
16 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Udongo wenye mboleo akaugeuza kuwa udongo usioweza kutoa, kwa sababu ya uovu wa wakaaji wake.


Wamisri wakawasukuma Waisraeli waondoke haraka, wakisema: “Hakika tutakufa sisi wote!”


Musiwaruhusu waishi katika inchi yenu wasiwasukume kutenda zambi mbele yangu. Maana kama mukitumikia miungu yao, hakika ile itakuwa mutego wa kuwanasa.


wakati nitakaponyoosha mukono wangu juu ya inchi ya Misri na kuwatoa Waisraeli kati yao. Halafu Wamisri watatambua kwamba mimi ni Yawe.”


Nitakinga watu wangu na mambo yatakayowapata watu wako. Mambo hayo yatafanyika kesho.’ ”


Mutu mubaya ananaswa kwa kosa lake, lakini mutu wa haki anaimba na kufurahi.


Jambo moja nililotambua linalokuwa baya zaidi kuliko kifo, ni mwanamuke ambaye moyo wake ni mutego na wavu, na mikono yake ni kama minyororo. Lakini anayemupendeza Mungu anamwepuka mwanamuke yule, lakini mwenye zambi ananaswa naye.


Lakini wewe hautaunganishwa nao katika mazishi, maana uliiharibu inchi yako, uliwaua watu wako. Wazao wa waovu wasahauliwe kabisa!


Amuka! Amuka na nguvu, ee mukono wa Yawe! Amuka kama ulivyofanya hapo zamani, nyakati za vizazi vilivyopita. Si wewe ndiwe uliyemukatakata yule nyama mukubwa Rahabu, ukamutoboa yule nyoka mukubwa wa kuogopesha?


Moabu imekwisha kuangamizwa, kilio chake kinasikilika mpaka Zoari.


Kwa rafla Babeli imeanguka na kuvunjikavunjika; muomboleze kwa ajili yake! Mulete dawa kwa kutuliza maumivu yake; labda utaweza kupona.


Feza yao wala zahabu yao havitaweza kuwaokoa katika siku hiyo ya kasirani ya Yawe. Kwa moto wa wivu wake dunia yote itateketezwa. Kwa ukamilifu na kwa namna ya kuogopesha atawafanya wakaaji wote katika dunia watoweke.


Maneno hayo ninayosema ni kwa faida yenu, wala si kwa kuwafungia njia. Ninataka kuwaonyesha namna ya kuishi sawa inavyofaa, kusudi mupate kumutumikia Bwana pasipo kizuizo chochote.


mujue kwa hakika kwamba Yawe, Mungu wenu, hataendelea kuyafukuza mataifa haya mbele yenu, lakini yatakuwa kwenu kikwazo na mutego. Yatakuwa kwenu mujeledi wa kuwapiga na miiba ya kuwachoma kwa macho mpaka pale mutakapoangamia na kutoka katika inchi hii nzuri ambayo Yawe, Mungu wenu, amewapa.


Saulo alifikiri: “Ngoja nitamutoa Mikali kusudi akuwe mutego kwake. Na bila shaka Wafilistini watamwua.” Hivyo Saulo akamwambia Daudi kwa mara ya pili: “Sasa nitakuwa baba mukwe wako.”


Kisha wakatuma ujumbe na kukusanya wakubwa wa Wafilistini na kuwaambia: “Mulirudishe Sanduku la Mungu wa Israeli kwa nafasi yake, kusudi lisituue sisi pamoja na watu wetu.” Walifanya hivyo kwa sababu kulikuwa hofu kubwa katika muji muzima kwa sababu Mungu alikuwa anawaazibu vikali.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ