Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Kutoka 10:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Ukikataa kuwaacha watu wangu waondoke, basi, kesho nitaleta nzige washambulie inchi yako.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Kutoka 10:4
15 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Basi, Musa na Haruni wakamwendea mufalme wa Misri na kumwambia: “Yawe, Mungu wa Waebrania, anasema hivi: ‘Mpaka wakati gani utakataa kujinyenyekeza mbele yangu? Uwaache watu wangu waondoke kusudi wanitumikie.


Inchi yote ya Misri itakuwa giza kwa sababu ya nzige wale. Watakula kila kitu kilichobaki nyuma ya ile mvua ya mawe. Vilevile hawataacha chochote juu ya miti inayoota katika mashamba.


Nami ninakuambia: Umwache mwana wangu aondoke, kusudi anitumikie! Kama ukikataa kumwachilia aondoke, angalia nitamwua muzaliwa wako wa kwanza mwanaume.’ ”


Kisha, Musa na Haruni wakamwendea mufalme wa Misri, wakamwambia: “Yawe, Mungu wa Israeli anasema hivi: ‘Uwaache watu wangu waondoke, wanifanyie sikukuu katika jangwa.’ ”


Watu wakawakusanya vyura wale malundomalundo. Inchi nzima ikanuka.


Tusafiri mwendo wa siku tatu katika jangwa tumutolee Yawe, Mungu wetu, sadaka kama vile atakavyotuamuru.”


Kwa hiyo kesho, wakati kama huu, nitaleta mvua kubwa ya mawe ambayo haijatokea katika inchi ya Misri, tangu mwanzo wake mpaka leo.


Tena, Yawe akaweka wakati akisema: “Kesho mimi Yawe nitatimiza jambo hilo katika inchi ya Misri.”


nzige hawana mufalme, lakini wote wanaenda pamoja kwa vikundi;


Nitawarudishia miaka ile iliyokuliwa na nzige, kila kitu kilichokuliwa na tunutu, parare na panzi, hilo kundi kubwa nililowaletea!


Mutapanda mbegu nyingi lakini mutavuna kidogo tu kwa sababu nzige watakula mazao yenu.


Nzige wakatokea katika ule moshi, na kusambaa juu ya dunia. Nao wakapewa nguvu zinazokuwa kama za nge.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ