Basi, Musa na Haruni wakamwendea mufalme wa Misri na kumwambia: “Yawe, Mungu wa Waebrania, anasema hivi: ‘Mpaka wakati gani utakataa kujinyenyekeza mbele yangu? Uwaache watu wangu waondoke kusudi wanitumikie.
Inchi yote ya Misri itakuwa giza kwa sababu ya nzige wale. Watakula kila kitu kilichobaki nyuma ya ile mvua ya mawe. Vilevile hawataacha chochote juu ya miti inayoota katika mashamba.
Kisha, Musa na Haruni wakamwendea mufalme wa Misri, wakamwambia: “Yawe, Mungu wa Israeli anasema hivi: ‘Uwaache watu wangu waondoke, wanifanyie sikukuu katika jangwa.’ ”