18 Basi, Musa akaondoka kwa mufalme, akaenda kumwomba Yawe.
Naye Yawe akaleta upepo mukali toka upande wa magaribi, ukawainua wale nzige na kuwasukumia kwenye bahari Nyekundu. Hakuna hata nzige mumoja aliyebaki katika inchi nzima ya Misri.
Kisha, Yawe akamwambia Musa: “Umwambie Haruni ainue fimbo yake na kupiga mavumbi, nayo yatageuka kuwa chawa katika inchi yote ya Misri.”
Basi, Musa na Haruni wakaondoka kwa nyumba ya mufalme wa Misri na Musa akamulilia Yawe amwondolee mufalme vyura wale aliomuletea.
Yawe akafanya kama vile Musa alivyomwomba. Vyura wakakufa katika nyumba, viwanja na kwenye baraza za nyumba na katika mashamba.
Watu wakamulilia Musa, naye akamwomba Yawe na moto huo ukazimika.
Lakini mimi ninawaambia: muwapende waadui zenu na muwaombee wale wanaowatesa.
Muwaombee baraka wale wanaowalaani. Muwaombee wale wanaowaonea.