Kutoka 10:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
10 Mufalme wa Misri akawaambia: “Basi, Yawe akuwe pamoja nanyi kama nitawaruhusu mujiendee na watoto wenu. Ni wazi kwamba muko na nia mbaya ndani ya moyo wenu.
Musidanganywe na Hezekia wala musishawishiwe kwa hayo. Musimwamini mutu huyu, kwa maana hakujatokea mungu wa taifa au mufalme yeyote aliyeweza kuwakomboa watu wake kutoka mikono ya mufalme wa Asuria. Vile vile mungu wenu hataweza!”
Kisha, mufalme wa Misri akamwita Musa, akamwambia: “Mwende mumutumikie Yawe. Watoto wenu vilevile wanaweza kwenda pamoja nanyi. Lakini kondoo na mbuzi, na ngombe wenu wabaki.”
Musa akamujibu: “Kila mutu, vijana na wazee, tutaondoka na watoto wetu wanaume na wanawake, kondoo na mbuzi wetu na ngombe. Kwa maana tunapaswa kumufanyia Yawe sikukuu.”
Muchana, Yawe aliwatangulia katika munara wa wingu kwa kuwaonyesha njia. Na usiku aliwatangulia katika munara wa moto kuwaangazia, kusudi waweze kusafiri muchana na usiku.