Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Kutoka 1:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Lakini wazao wa Israeli wakaongezeka sana, wakakuwa wengi na wenye nguvu sana, wakaenea kila pahali katika inchi ya Misri.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Kutoka 1:7
29 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mungu akasema: “Maji yajae makundi ya viumbe vyenye uzima. Na ndege waruke katika anga.”


Mungu akawabariki na kuwaambia: “Muzae, muongezeke, na mujaze inchi na kuitawala. Mutawale samaki wa bahari, ndege wa anga, na kila kiumbe chenye uzima kinachotembea katika dunia.”


Nitakufanya wewe kuwa taifa kubwa, nitakubariki na kutukuza jina lako, nawe utakuwa baraka.


Wazao wako nitawafanya wakuwe wengi wasihesabike, kama vile mavumbi ya inchi. Kama vile vumbi isivyoweza kuhesabika, ndivyo wazao wako hawataweza kuhesabika!


Yawe akamupeleka Abramu inje na kumwambia: “Angalia mbinguni! Uhesabu nyota, kama kweli utaweza kuzihesabu! Hivi ndivyo wazao wako watakavyokuwa wengi!”


Nitamubariki, naye atakuzalia mutoto mwanaume. Nitamubariki Sara, naye atakuwa mama wa mataifa mengi na wafalme wa mataifa watatoka kwake.”


hakika nitakubariki, na wazao wako nitawazidisha kama nyota mbinguni na kama muchanga pembeni ya bahari. Wazao wako watarizi miji ya waadui zao.


Kisha Isaka akakwenda pahali pengine na kuchimba kisima kingine. Lakini hicho hawakukigombania. Hivyo Isaka akakiita “Nafasi Pana”, akisema: “Sasa Yawe ametuachia nafasi, nasi tutastawi katika inchi hii.”


Nitawazidisha wazao wako wakuwe kama nyota za mbinguni na kuwapa inchi hizi zote. Kutokana na wazao wako, mataifa yote katika dunia yatabarikiwa,


Wazao wako watakuwa wengi kama mavumbi ya dunia, na urizi wao utaenea kila pahali: upande wa magaribi, mashariki, kaskazini na kusini. Kwa njia yako na ya wazao wako, jamaa zote katika dunia zitabarikiwa.


Tena Mungu akamwambia: “Mimi ni Mungu Mwenye Nguvu. Ujaliwe wazao wengi na kuongezeka. Taifa na kundi la mataifa watatokea kwako na wafalme watatokea katika uzao wako.


Mungu akamwambia: “Mimi ni Mungu, Mungu wa baba yako. Usiogope kwenda Misri. Utakapokuwa kule, nitakufanya kuwa taifa kubwa.


Basi, watu wa Israeli wakakaa katika eneo la Goseni katika inchi ya Misri. Wakiwa kule, wakapata mali nyingi, wakazaa na kuongezeka sana.


na malaika ambaye aliniokoa katika mabaya yote, awabariki vijana hawa! Jina langu na majina ya babu zangu, Abrahamu na Isaka, yadumishwe katika vijana hawa; nao waongezeke kwa wingi katika dunia.”


Akaniambia: ‘Nitakufanya ukuwe na wazao na uongezeke. Nitakufanya ukuwe babu ya jamii kubwa za watu. Inchi hii nitawapa wazao wako, wairizi milele.’ ”


Mungu akamubariki Noa na wana wake, akiwaambia: “Muzae, muongezeke, mujaze inchi.


Ukafanya wazao wao kuwa wengi kama nyota za mbinguni; ukawaleta katika inchi uliyowaahidi babu zao.


Yawe akawafanya watu wake wazae sana; akawajalia nguvu kuliko waadui zao.


Aliwabariki watu wake, wakaongezeka; na hesabu ya wanyama wao akaizidisha.


Lakini kadiri walivyoteswa ndivyo Waisraeli walivyozidi kuongezeka na kuenea katika inchi. Hivyo Wamisri wakawaogopa sana watu wa Israeli.


Waisraeli waliondoka katika muji wa Ramesesi, wakasafiri kwa miguu kuelekea Sukoti. Walikuwa wanaume yapata elfu mia sita, bila kuhesabu wanawake na watoto.


Tena mufalme akasema: “Hawa watu ni wengi nanyi munataka waache kufanya kazi!”


Uishi, na ukomae kama mumea katika shamba. Nawe ukakomaa na kurefuka hata ukakuwa binti. Maziba yako yakakomaa na nywele zako nazo zikarefuka. Lakini ulikuwa uchi kabisa.


Mungu wa taifa hili la Waisraeli aliwachagua babu zetu, naye akawafanya kuwa taifa kubwa walipokuwa wakikaa kama wageni katika inchi ya Misri. Kisha akawaondosha kule kwa uwezo wake mukubwa


Babu zenu walipokwenda Misri, walikuwa watu makumi saba tu, lakini sasa Yawe, Mungu wenu, amewafanya kuwa wengi kama nyota mbinguni.


utasema maneno haya mbele ya Yawe, Mungu wako: ‘Baba yangu alikuwa Musuria aliyetangatanga huko na huko, kisha akashuka kwenda Misri akaishi huko kama mugeni. Yeye na jamaa yake walikuwa watu wachache tu walipokuwa huko, lakini wakakuwa taifa kubwa lenye nguvu na watu wengi.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ