Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Kutoka 1:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 Basi, Wamisri wakachagua wakubwa wawasimamie Waisraeli na kuwatesa kwa kazi ngumu. Waisraeli wakafanya kazi ya kumujengea mufalme wa Misri miji ya kuwekea akiba, Pitomu na Ramesesi.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Kutoka 1:11
21 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yawe akamwambia Abramu: “Ujue hakika kwamba wazao wako watakaa kama wageni katika inchi isiyokuwa yao, watakuwa watumwa na watateswa kwa muda wa miaka mia ine.


Basi, Yosefu akawapa baba yake na wandugu zake eneo la Ramesesi lililokuwa bora kabisa katika inchi ya Misri, likuwe makao yao, nao wakalirizi kama vile mufalme alivyoagiza.


na miji yake yote ya kuwekea akiba, magari yake ya vita, na waaskari wapanda-farasi wake; vilevile na chochote alichotaka kujenga katika Yerusalema, Lebanoni au nafasi ingine katika ufalme wake.


Hapo mufalme Beni-Hadadi akakubali pendekezo la mufalme Asa. Akawatuma majemadari wake na majeshi yake kwenda kushambulia miji ya Israeli. Nao wakateka miji ya Iyoni, Dani, Abeli-Maimu, na miji yote ya Nafutali iliyokuwa na hazina.


na kuujenga muji wa Tadimori katika jangwa. Alijenga upya miji ya gala iliyokuwa kule Hamati.


Walitangatanga kutoka taifa mpaka taifa, kutoka inchi moja mpaka inchi ingine.


Wimbo wa safari za kidini. Kila mutu katika Israeli aseme: “Nimesumbuliwa vibaya tangu ujana wangu”.


Nimesumbuliwa vibaya tangu ujana wangu, lakini hawakunishinda.


“Wafalme na majeshi yao wanakimbia ovyo!” Wanawake waliobaki ndani ya nyumba waligawanya vitu vilivyonyanganywa,


Aliwapa watu wa Israeli agizo hilo, aliposhambulia inchi ya Misri. Ninasikia sauti nisiyoitambua ikisema:


Wakayafanya maisha yao kuwa magumu kwa kazi ngumu ya kutengeneza chokaa na kufyatua matofali, na kazi zote za shamba. Katika kazi zile zote, Waisraeli walitumikishwa kwa kinguvu.


Siku moja, Musa alipokuwa mutu muzima, akawaendea Waebrania wenzake kwa kujionea taabu zao. Basi, akamwona Mumisri mumoja akimupiga Mwebrania, mumoja wa wandugu zake.


Kisha Yawe akamwambia: “Nimeona mateso ya watu wangu wanaokuwa katika inchi ya Misri na nimesikia kilio chao kinachosababishwa na watesaji wao. Ninajua mateso yao,


Basi, wakubwa na wasimamizi wa watu wakatoka na kuwaambia watu: “Mufalme wa Misri anasema hivi: ‘Sitawapa nyasi.


Halafu wasimamizi wa Waisraeli wakamwendea mufalme, wakamulilia wakisema: “Kwa nini unatutendea hivi sisi watumishi wako?


Lakini hesabu ya matofali yanayotengenezwa kila siku ikuwe ileile, wala kusipunguke hata tofali moja, kwa sababu watu hawa ni wavivu ndio maana wanapiga kelele na kusema: ‘Utuache tuende kutoa sadaka kwa Mungu wetu.’


Kasirani ni kali na hasira inaangamiza; lakini ni nani anayeweza kupingana na wivu?


Jinsi babu zetu walivyokwenda Misri, ambako tuliishi kwa muda murefu na jinsi Wamisri walivyowatesa babu zetu, wakatutesa na sisi vilevile.


Wamisri walitutendea kwa ukali wakatutesa na kutulazimisha kufanya kazi ngumu ya watumwa.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ