Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Kumbukumbu la Sheria 17:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 na huko mutawaendea makuhani wa Kilawi, na mwamuzi ambaye yuko katika kazi kwa wakati huo, nanyi mutatoa mashitaki kwao nao watawatangazia uamuzi wao.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Kumbukumbu la Sheria 17:9
15 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kati ya watu wa ukoo wa Isiari, Kenania na wana wake walipewa kazi za utawala kama kusimamia watu na waamuzi, kwa ajili ya Waisraeli.


Wakiwa na ugomvi wowote wao wanakuja kwangu nami ninaamua kati ya mutu na mwenzake na kuwafundisha masharti ya Mungu na maamuzi yake.”


Kukitokea ubishi juu ya ngombe, au punda, au kondoo, au nguo, au kitu chochote kilichopotea ambacho kila mumoja anadai kwamba ni chake, wale wanaobishana wataletwa mbele ya Mungu. Yule ambaye Mungu ataamua kwamba amekosa, atamulipa mwenzake mara mbili.


Kisha, watu wakasema: Tuende tufanye shauri baya juu ya Yeremia, maana hatukosi makuhani wa kutufundisha. Vilevile hatukosi watu wenye hekima wa kutushauria na manabii wa kututangazia ujumbe wa Mungu! Mukuje tumushitaki kufuatana na maneno yake mwenyewe, wala tusiyatilie maana mambo yote anayosema.


Kukikuwa magombano wataamua kadiri ya maamuzi yangu. Katika sikukuu zote watafuata sheria zangu na maamuzi yangu, na kuzitakasa Sabato zangu.


Yawe wa majeshi anasema hivi: Makuhani watoe uamuzi juu ya jambo hili:


Yawe wa majeshi anasema hivi: Ukifuata njia zangu na kushika maagizo niliyokupa, basi, utaisimamia nyumba yangu na viwanja vyake. Nami nitakuwezesha kuingia katika utumishi wangu kama hawa wanaosimama mbele yangu.


na kuwauliza makuhani wa hekalu la Yawe wa majeshi maneno haya: Tuendelee kuomboleza na kufunga kula chakula katika mwezi wa tano kama tulivyofanya kwa muda wa miaka mingi sasa?


Ni kazi ya makuhani kuwafundisha watu maarifa ya kweli juu ya Mungu kusudi watu wawaendee kwa kujifunza mapenzi yangu kwao, maana makuhani ni wajumbe wa Yawe wa majeshi.


“Mutachagua waamuzi na wakubwa kutoka makabila yenu katika miji yenu ambayo Yawe, Mungu wenu, atawapa nao watatoa hukumu za haki kwa watu.


Kisha mutafanya kama vile watakavyowatangazia pale pahali Yawe atakapochagua. Mutakuwa waangalifu kufanya yote kama vile watakavyowaagiza.


Nao makuhani wa ukoo wa Lawi sharti wakuwe pale. Yawe, Mungu wenu, aliwachagua wamutumikie na kubariki kwa jina lake. Wao vilevile ndio wenye mamlaka ya kuamua magomvi na maneno juu ya kuumizana.


“Ikiwa kuna ugomvi kati ya watu wawili, na wakienda kwa tribinali kuamua maneno yao, mumoja akionekana hana kosa, na mwingine akihukumiwa,


Na watafundisha wazao wa Yakobo maagizo yako; watafundisha watu wa Israeli sheria yako. Walawi watafukiza ubani mbele yako, sadaka nzima za kuteketezwa juu ya mazabahu yako.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ