Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Kumbukumbu la Sheria 13:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 “Kukitokea nabii au mutabiri wa kutumia ndoto kati yenu na kuwapatia kitambulisho au ajabu fulani,

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Kumbukumbu la Sheria 13:2
16 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mutu huyo akaonyesha kitambulisho siku ileile, akasema: “Hiki ndicho kitambulisho Yawe alichosema: ‘Mazabahu hii itabomoka, na majivu yanayokuwa juu yake yatamwangika.’ ”


Anayemutolea mungu mwingine sadaka pahali pa Yawe pekee, lazima aangamizwe kabisa.


Lakini wachawi wa Misri kwa kutumia uchawi wao wakafanya vivyo hivyo. Kwa hiyo moyo wa mufalme wa Misri ukabaki kuwa mugumu, naye hakuwasikiliza Musa na Haruni. Ikakuwa kama vile Yawe alivyokuwa amesema.


Vilevile mimi Yawe ninasema kwamba nitawashambulia manabii wanaotabiri ndoto zao za uongo kwa watu wangu, na kuwapotosha kwa uongo wao na upuuzi wao. Mimi sikuwatuma wala kuwaamuru waende, kwa hiyo hawatawafalia watu hao kitu. –Ni ujumbe wa Yawe!


Basi, ninyi musiwasikilize manabii wenu, wapiga ramuli wenu, wafasiriaji wenu wa ndoto, waaguzi wenu au wachawi wenu, wanaowaambia kwamba musimutii mufalme wa Babeli.


Lakini nabii anayetabiri maneno ya amani, anaweza kutambulikana kama ni nabii aliyetumwa na Yawe, wakati mambo aliyotabiri yanapotokea.


Sanamu zao za kupigia ramuli ni uongo mutupu, na waaguzi wao wanaagua uongo; watabiri wao wanatabiri ndoto danganyifu, na kuwapa watu faraja za bure. Ndiyo maana watu wa Yuda wanatangatanga kama kondoo; wanataabika maana wamekosa muchungaji.


kwa maana kutatokea watu wanaojiita kwa uongo ‘Kristo’ pamoja na manabii wa uongo, nao wataonyesha vitambulisho vikubwa na maajabu, hata ikiwezekana, wawadanganye hata watu waliochaguliwa na Mungu.


“Mutakapoishi katika miji ambayo Yawe, Mungu wenu anawapa, labda mutasikia


Lakini nabii huyo au mutabiri wa kutumia ndoto atauawa, kwa sababu atakuwa amewafundisha uasi mbele ya Yawe, Mungu wenu, aliyewatoa katika inchi ya Misri na kuwakomboa kutoka katika utumwa, kusudi muache njia ambayo Yawe, Mungu wenu, aliwaamuru kufuata. Hivi ndivyo mutakavyokomesha uovu kati yenu.


Lakini nabii yeyote atakayesema kwa jina la miungu mingine, au atakayejaribu kusema neno kwa jina langu wakati mimi sikumwambia aseme, huyo nabii atakufa.’


Kama nabii akisema kitu aseme ni kwa jina la Yawe, na kitu hicho hakifanyiki au hakiko kweli, jambo hilo Yawe hakulisema; nabii amelisema kwa kiburi, nanyi musitishwe na jambo hilo.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ