Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Kumbukumbu la Sheria 11:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 mupate kuishi kwa muda murefu katika inchi inayotiririka maziwa na asali, inchi ambayo Yawe aliahidi kuwapa babu zenu na wazao wao.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Kumbukumbu la Sheria 11:9
19 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

na hivyo, nimeshuka kusudi niwaokoe toka mikono ya Wamisri. Nitawatoa katika inchi na kuwapeleka katika inchi nzuri na kubwa, inchi inayotiririka maziwa na asali, inchi ya Wakanana, Wahiti, Waamori, Waperizi, Wahivi na Wayebusi.


Kwa hiyo mushike masharti yake na amri zake ambazo ninawapa leo kusudi mufanikiwe, ninyi pamoja na wazao wenu, na kuishi siku nyingi katika inchi ambayo Yawe, Mungu wenu, anawapa ikuwe yenu milele.”


Wakati wote munapokuwa wazima, mutapaswa kumwogopa Yawe, Mungu wenu, na kutii masharti yote na amri ninazowapa ninyi na wazao wenu kusudi mupate kuishi maisha marefu.


Siku hiyo niliwaapia kwamba nitawatoa katika inchi ya Misri na kuwapeleka mpaka kwenye inchi niliyowachagulia, inchi ya maziwa na asali na inchi nzuri kuliko inchi zote.


Munaweza kuirizi inchi yao si kwa sababu ninyi ni watu wa haki wenye mioyo ya usawa; lakini Yawe, Mungu wenu, anawafukuza watu hao mbele yenu kwa sababu ni waovu na anataka kuweka imara lile neno alilowaapia babu zenu, Abrahamu, Isaka na Yakobo.


“Uheshimu baba yako na mama yako, kama vile mimi Yawe, Mungu wako, nilivyokuamuru, kusudi uishi maisha marefu na kufanikiwa katika inchi ninayokupatia mimi Yawe, Mungu wako.


Kumwogopa Yawe kunarefusha maisha, lakini miaka ya waovu itakuwa mifupi.


Kwa musaada wangu mimi Hekima siku zako zitaongezwa; utaongezewa miaka mingi katika maisha yako.


Maana vitakupa wingi wa siku, maisha marefu na fanaka kwa wingi.


Mufanye yale yanayomupendeza Yawe, kusudi mupate kufanikiwa. Mutaweza kuirizi inchi ile nzuri ambayo Yawe aliapa kuwapa babu zenu,


Uwaheshimu baba yako na mama yako, kusudi uishi maisha marefu katika inchi ninayokupatia mimi Yawe, Mungu wako.


Mutafuata njia yote Yawe, Mungu wenu, aliyowaamuru kufuata kusudi mambo yenu yawaendekee vizuri na mupate kuishi muda murefu katika inchi mutakayotwaa ikuwe mali yenu.


Yawe, Mungu wenu, anawaleta kwenye inchi nzuri, inchi yenye vijito na chemichemi, na maji yanayobubujika kutoka bonde na milima;


Inchi munayokwenda kurizi si kama inchi ya Misri mulikotoka, ambako mulipanda ngano nanyi mulipaswa kuleta maji kutoka kwenye mito kwa kuimwangilia kama vile mulivyofanya kwa mashamba ya mboga.


Inchi hii yote nimeiweka mbele yenu. Basi, muende kutwaa inchi hiyo ambayo mimi Yawe niliapa kuwapa wazee wenu Abrahamu, Isaka, Yakobo na wazao wao.’ ”


Kwa hiyo enyi Waisraeli, mukuwe waangalifu kwa kuzitimiza, kusudi mufanikiwe na kuongezeka sana katika inchi hiyo inayotiririka maziwa na asali kama vile alivyowaahidi.


kusudi ninyi na watoto wenu mupate kuishi maisha marefu katika inchi ambayo Yawe, Mungu wenu, aliapa kuwapa babu zenu, siku zote mbingu zitakapodumu juu ya dunia.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ