Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 9:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Kuta za matofali zimeanguka lakini sisi tutazijenga kwa mawe yaliyochongwa! Nyumba za nguzo za mikuyu zimeharibiwa lakini pahali pake tutajenga za mierezi.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 9:9
23 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mikaya akamujibu: “Siku utakapoingia katika chumba cha ndani kwa kujificha, ndipo utakapojua.”


Kiburi kinatangulia maangamizi; majivuno yanatangulia maanguko.


Ee Yawe umeinua mukono kwa kuwaazibu, lakini hawauoni. Uwaonyeshe namna unavyowapenda watu wako nao watapata haya. Moto unaowatayarishia waadui zako, uwateketeze!


Ole wa Samaria, muji unaokuwa kama taji juu ya bonde kwenye udongo muzuri. Walevi wa ajabu wa Efuraimu wanajivuna kwa ajili yake, lakini utukufu wake utatoweka kama ua linalonyauka!


Majivuno na utukufu wa walevi wa Efuraimu vitakanyagwakanyagwa chini,


Musikilize, enyi wenye vichwa vigumu, munisikilize enyi munaokuwa mbali na ukombozi.


Lakini nilikujua wewe kuwa na moyo mugumu; kichwa kigumu kama chuma, uso wako kama shaba.


Mufalme wa Yuda alipopata habari kwamba Waaramu wanashirikiana na Waisraeli, yeye pamoja na watu wote wa Yuda waliogopa na kutetemeka kama miti inayotikiswa na upepo.


Watu wote watatambua, ukoo wote wa Efuraimu na wakaaji wa Samaria. Kwa kiburi na majivuno wanasema:


Angalia, Wakaldea wamechimba mifereji kuuzunguka muji; wanauzunguka kusudi wapate kuuteka; wanaushambulia. Vita, njaa na magonjwa vitaufanya muji utekwe na watu hao. Kweli mambo uliyotabiri yametokea. Unaona mwenyewe.


Ndivyo nitakavyoiazibu Misri. Na watu watatambua kwamba mimi ni Yawe.


Lakini hayo unayosema yatakapotukia –nayo kweli yatatukia –basi, halafu watatambua kwamba nabii amekuwa kati yao.


Mufalme ataomboleza, mukubwa atakata tamaa na watu watatetemeka kwa hofu. Nitawatendea kufuatana na mienendo yao, nitawahukumu kama nilivyowahukumu wengine. Halafu watatambua kwamba mimi ni Yawe.


Sitawaachilia wala sitawaonea huruma. Nitawaazibu kulingana na mienendo yenu nayo machukizo yangali bado kati yenu. Halafu mutatambua kwamba ni mimi Yawe ninayewaangamiza.


Waisraeli wamemusahau Muumba wao, wakajijengea nyumba kubwa; watu wa Yuda wamejiongezea miji yenye kuzungukwa na kuta, lakini mimi nitatuma moto katika miji hiyo, na kuziteketeza kuta zao.


Waedomu, wale wazao wa Esau, wanasema kwamba ingawa miji yao imeharibiwa, watajenga upya mabomoko yake. Lakini, Yawe wa majeshi anasema hivi: Wanaweza kuijenga upya, lakini mimi nitaibomoa tena. Watu watawaita: Taifa ovu ambalo Yawe amelikasirikia milele.


Yawe anasema hivi: Maneno yenu yamekuwa muzigo kwangu. Hata hivyo munasema: Tumesema nini juu yako?


Na hivi vilevile, ninyi vijana, munapaswa kuwatii hao wazee. Ninyi wote munapaswa kuwa na unyenyekevu, mupate kutumikiana; maana Maandiko Matakatifu yanasema: “Mungu anawapinga wenye kiburi, lakini anawajalia wanyenyekevu neema.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ