Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 9:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Utawala wake utastawi siku zote, amani ya ufalme wake haitakoma. Atakamata madaraka ya mufalme Daudi na kutawala juu ya ufalme wake; ataustawisha na kuuimarisha kwa kufuata sheria ya Mungu na kutenda kwa haki tangu sasa na hata milele. Yawe wa majeshi atafanya mambo hayo.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 9:6
82 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yeye ndiye atakayejenga nyumba kwa ajili ya jina langu na kiti chake cha kifalme cha ufalme wake nitakiimarisha milele.


Ukoo wako na ufalme wako vitadumu imara siku zote. Kiti chako cha kifalme kitakuwa imara milele.”


Asifiwe Yawe, Mungu wako, ambaye amependezwa nawe, akakuweka juu ya kiti cha kifalme cha Israeli! Kwa sababu Yawe anapenda Israeli milele, amekuweka wewe ukuwe mufalme, kusudi uimarishe haki na sheria ya Mungu.”


Azabu ya mauaji hayo itakuwa juu ya Yoabu na wazao wake milele. Lakini Yawe atawabariki siku zote Daudi na wazao wake watakaoikalia kiti chake cha kifalme.”


Lakini mimi atanibariki, na kiti cha kifalme cha Daudi kitaimarishwa mbele ya Yawe milele.”


Kwa hiyo, ee Mungu wetu, Mungu mukubwa, mwenye nguvu na wa kutisha, wewe unashika agano lako na kutenda wema. Mateso yaliyotupata, sisi, wafalme wetu, wakubwa wetu, makuhani wetu, manabii wetu, babu zetu na watu wako wote tangu wakati wa wafalme wa Asuria mpaka leo, usiyaone kuwa ni madogo.


Wewe ni muzuri kuliko wanadamu wote, maneno yako ni rehema tupu, Mungu amekubariki milele.


Mishale yako ni mikali, inapenya mioyo ya waadui za mufalme; nayo mataifa yanaanguka chini yako.


Kiti chako cha kifalme ni imara, kinadumu milele kama cha Mungu. Wewe unatawala watu wako kwa haki.


Zaburi ya Asafu. Mungu, Mungu Yawe, amesema, amewaita wakaaji wa dunia, tokea magaribi mpaka mashariki.


Jina la mufalme litukuzwe siku zote; utukufu wake udumu muda wote jua litakapokuwa. Kwake mataifa yote yabarikiwe; watu wote wamwite mwenye heri!


Milima ilete ustawi kwa watu wako, vilima vijae haki.


Haki istawi maisha yake yote, na amani kwa wingi mpaka mwezi ukome.


Hakika yeye ni tayari kuwaokoa wanaomuheshimu, na utukufu wake utadumu katika inchi yetu.


‘Siku zote nitamuweka mumoja wa wazao wako kuwa mufalme, tena nitaudumisha ufalme wako milele.’ ”


Nilifanywa kwa mwanzo wa nyakati, nilikuwa niko mbele ya dunia kuanza.


Wazao wa Yakobo wachache watakaobaki watamurudilia Mungu Mukubwa.


Haki itakuwa kama mukaba wa kujifunga, uaminifu utakuwa kama mukaba kwenye kiuno chake.


Kisha utawala wa wema utazinduliwa katika hema ya Daudi. Mutawala atakuwa mwaminifu. Atahukumu kufuatana na sheria ya Mungu, atakuwa mwepesi wa kutenda kwa haki.


Wewe, ee Yawe, umetupatia amani; umefanikisha shuguli zetu zote.


Ee Mungu, unawaweka katika amani wanaokuwa imara, unawaweka katika amani kwa sababu wanakutegemea.


Ujuzi huu nao unatoka kwa Yawe wa majeshi. Mipango yake ni ya ajabu, hekima yake ni kamilifu kabisa.


Kutatokea mufalme atakayetawala kwa haki, nao wakubwa wataongoza kwa kufuatana na sheria ya Mungu.


Maana kutakuwa watu watakaobaki kule Yerusalema; kule kwenye mulima Sayuni kutakuwa watu wachache watakaobakia. Yawe wa majeshi amekusudia kukamilisha hayo.


Yawe alipenda kumuponda kwa mateso. Alitoa uzima wake kwa ajili ya kuondoa zambi. Mutumishi wa Mungu atakuwa na wazao; ataishi maisha marefu. Yeye ndiye atakayetimiza mupango wa Yawe.


Maana, mbele ya Yawe, mutumishi wake alikomaa kama kichipukizi, kama muzizi katika inchi kavu. Hakukuwa na umbo wala sura ya kupendeza, wala hakukuwa na uzuri wowote wa kutuvuta.


Lakini aliumizwa kwa sababu ya zambi zetu, alipondwa kwa sababu ya maovu yetu. Kwa kuazibiwa kwake sisi tumepata uzima; kwa kupigwa kwake sisi tumepona.


Maana wewe ndiwe Baba yetu; Abrahamu, babu yetu, hatujali, naye Israeli hatutambui; lakini wewe, ee Yawe, ni Baba yetu. Wewe umeitwa tangu zamani: Mukombozi wetu.


Maana Yawe anasema hivi: Nitakuletea fanaka nyingi kama muto, utajiri wa mataifa kama muto uliofurika. Nanyi mutanyonya na kubebwa kama mutoto muchanga, mutabembelezwa kama mutoto juu ya magoti ya mama yake.


Basi, Bwana mwenyewe atawapa kitambulisho: bikira atapata mimba, atazaa mutoto mwanaume na kumwita jina lake “Emanueli – Mungu Yuko Pamoja Nasi”.


Mimi pamoja na watoto Yawe alionipa ni kitambulisho na mufano katika Israeli kwa jina la Yawe wa majeshi anayekaa kwenye mulima Sayuni.


Utasitasita mpaka wakati gani, ewe binti usiyekuwa mwaminifu? Maana, mimi nimefanya kitu kipya katika dunia; mwanamuke anamulinda mwanaume.


Wakati wa wafalme wale, Mungu wa mbinguni ataanzisha ufalme ambao hautaangamizwa hata kidogo. Watu wengine hawataushinda na kuutawala ufalme huo, lakini ufalme huo utaziponda na kuzikomesha falme zilizotangulia, nao utadumu milele.


Akapewa mamlaka, utukufu na ufalme, kusudi watu wa makabila yote, mataifa yote na luga zote wamutumikie. Utawala wake ni wa milele na ufalme wake hautaangamizwa hata kidogo.


Nyumba mupya itakuwa yenye utukufu zaidi kuliko ile ya kwanza. –Ni Yawe wa majeshi anayesema hivyo! Kutoka hapa nitawapa watu wangu fanaka. –Ni ujumbe wa Yawe wa majeshi!


Haya ni majina ya babu za Yesu Kristo, wa uzao wa Daudi, wa uzao wa Abrahamu. Abrahamu alizaa Isaka, Isaka alizaa Yakobo, Yakobo alizaa Yuda na wandugu zake, Yuda alizaa Peresi na Zera kutoka muke wake Tamari, Peresi alizaa Hesironi, Hesironi alizaa Ramu, Ramu alizaa Aminadabu, Aminadabu alizaa Nasoni, Nasoni alizaa Salmoni, Salmoni alizaa Boazi kutoka muke wake Rahaba, Boazi alizaa Obedi kutoka muke wake Ruta, Obedi alizaa Yese, Yese alizaa mufalme Daudi, Daudi alizaa Solomono (mama yake ndiye yule aliyekuwa muke wa marehemu Uria), Solomono alizaa Rehoboamu, Rehoboamu alizaa Abiya, Abiya alizaa Asa, Asa alizaa Yosafati, Yosafati alizaa Yoramu, Yoramu alizaa Uzia, Uzia alizaa Yotamu, Yotamu alizaa Ahazi, Ahazi alizaa Hezekia, Hezekia alizaa Manase, Manase alizaa Amoni, Amoni alizaa Yosia, Yosia alizaa Yekonia na wandugu zake, wakati Waisraeli walipohamishwa kwenda Babeli. Nyuma ya kuhamishwa kwa Waisraeli kwenda Babeli, Yekonia alizaa Saltieli, Saltieli alizaa Zerubabeli, Zerubabeli alizaa Abihudi, Abihudi alizaa Eliakimu, Eliakimu alizaa Azoro, Azoro alizaa Zadoki, Zadoki alizaa Akimu, Akimu alizaa Elihudi, Elihudi alizaa Eleazari, Eleazari alizaa Matani, Matani alizaa Yakobo, Yakobo alizaa Yosefu, yule alikuwa mume wa Maria, mama ya Yesu, anayeitwa Kristo.


“Angalia bikira atapata mimba, atazaa mutoto mwanaume, naye ataitwa Emanueli,” (maana yake “Mungu yuko pamoja nasi”).


“Baba yangu ameweka vitu vyote katika mikono yangu. Hakuna mutu anayemujua Mwana isipokuwa Baba, wala hakuna anayemujua Baba isipokuwa Mwana, na yeyote Mwana anayetaka kumujulisha kwake.


Kisha Yesu akakuja karibu nao, na kuwaambia: “Nimepewa mamlaka yote mbinguni na katika dunia.


Malaika akamujibu: “Roho Mutakatifu atakufikia, na uwezo wa Mungu Mukubwa utakufunika kama vile kivuli. Kwa sababu hii mutoto yule atakayezaliwa ataitwa Mutakatifu na Mwana wa Mungu.


Leo hii Mwokozi amezaliwa kwa ajili yenu katika muji wa Daudi, yeye ndiye Kristo na Bwana.


“Sifa kwa Mungu juu mbinguni, na amani katika dunia kwa watu anaowapenda.”


Kwa maana mimi mwenyewe nitawapa masemi na hekima hata waadui zenu hawataweza kuyapinga wala kuyakataa.


Neno alifanywa kuwa mutu, naye akaishi kati yetu, akijaa neema na ukweli. Tuliona utukufu wake, utukufu ule Mwana wa pekee aliopewa na Baba.


Sisi wote tumepokea sehemu ya neema aliyojaa nayo, akitupatia baraka nyingi sana.


“Ninawaachia amani; ninawapa amani yangu. Siwapatii ninyi amani hii kama dunia inavyoitoa. Musifazaike wala musiogope.


Yeye ametuma ujumbe wake kwa Waisraeli, akiwahubiri Habari Njema ya amani kwa njia ya Yesu Kristo, anayekuwa Bwana wa watu wote.


Mujichunge ninyi wenyewe na muchunge vilevile lile kundi lote Roho Mutakatifu alilowapatia kusudi mukuwe wasimamizi wao. Hivi mutaweza kuchunga kanisa la Mungu ambalo alijipatia kwa damu ya Mwana wake.


Yeye hakumwacha Mwana wake wa pekee, lakini alimutoa kwa ajili yetu sisi wote. Namna gani atakosa kutupatia vilevile vitu vyote kwa njia ya mwana wake?


Wao ni wazao wa babu zetu, na Kristo alizaliwa kimwili katika kizazi chao. Yeye ndiye mukubwa kupita wote na Mungu anayesifiwa kwa milele! Amina.


Lakini Mungu amewaunganisha na Yesu Kristo, naye amemufanya Kristo kuwa hekima yetu. Kwa njia ya Kristo tunahesabiwa haki mbele ya Mungu, tumekuwa watu watakatifu wa Mungu, na kukombolewa toka zambi zetu.


Kwa maana Kristo anapaswa kutawala mpaka atakapowashinda waadui zake wote na kuwaweka chini ya miguu yake.


Ndiyo kusema, Mungu ndiye aliyekuwa akipatanisha watu wote na yeye mwenyewe kwa njia ya Kristo bila kuhesabu makosa yao. Yeye ametupatia ujumbe wa upatanisho.


Maana Yawe, Mungu wenu, ndiye Mungu wa miungu na Bwana wa wabwana. Yeye ni Mungu mukubwa na mwenye nguvu, na wa kuogopesha. Hapendelei wala hapokei kituliro.


kwa maana hazina zote za hekima na elimu zimefichwa ndani yake.


Hakika siri ya ibada yetu ni kubwa: Yeye alitokea kwa mufano wa mutu, alishuhudiwa na Roho Mutakatifu kuwa mwenye haki. Alionekana na wamalaika. Alitangazwa katikati ya mataifa. Aliaminiwa popote katika dunia. Na alinyanyuliwa mbinguni katika utukufu.


Na hivi tutaishi tukingojea ule uheri tunaoutumainia, wakati utukufu wa Mungu wetu Mukubwa na Mwokozi wetu Yesu Kristo utakapotokea.


Lakini juu ya Mwana, Mungu alisema: “Kiti chako cha kifalme, Ee Mungu, kitadumu hata milele. Unatawala ufalme wako kwa haki.


Mungu wa amani, aliyemufufua Bwana wetu Yesu ambaye ni Muchungaji mukubwa wa kondoo kwa njia ya kumwanga damu yake inayohakikisha agano la milele,


Tunajua vilevile kwamba Mwana wa Mungu amekwisha kuja, naye ametupatia ufahamu tupate kumujua Mungu anayekuwa wa kweli. Nasi tunaungana na yule Mungu anayekuwa wa kweli kwa njia ya Mwana wake Yesu Kristo. Huyu ndiye Mungu wa kweli na uzima wa milele.


Na juu ya nguo yake na paja la muguu wake kulikuwa kumeandikwa jina hili: “Mufalme wa wafalme na Bwana wa wabwana.”


Malaika wa Yawe akamujibu: “Kwa nini unataka kujua jina langu? Ni la ajabu.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ