Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 9:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Maana mutoto amezaliwa kwa ajili yetu, tumepewa mutoto mwanaume. Naye atapewa mamlaka ya kutawala. Ataitwa: “Mushauri wa Ajabu”, “Mungu Mwenye Nguvu”, “Baba wa Milele”, “Mufalme wa Amani”.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 9:5
29 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Halafu Yakobo akamwambia: “Tafazali, ninakuomba uniambie jina lako.” Lakini yeye akamwambia: “Kwa nini kuniuliza jina langu?” Kisha akamubariki Yakobo.


Mukuje muone matendo ya Yawe. Muone maajabu aliyofanya katika dunia.


Milima ilete ustawi kwa watu wako, vilima vijae haki.


Musikilize na kutii maneno atakayosema, wala musimwasi. Hatawasamehe uasi wenu maana nimemutuma kwa jina langu.


Musikilize kelele kwenye milima kama za kundi kubwa la watu! Musikilize kelele za falme, na mataifa yanayokusanyika! Yawe wa majeshi analichunguza kundi linalokwenda kwa vita.


Mungu atafanya hukumu kati ya mataifa; ataamua maneno kati ya watu wengi. Watu watafua panga za vita kuwa majembe na mikuki yao kuwa visu vya kuvuna. Taifa halitapigana na taifa lingine wala hayatafanya tena mazoezi ya vita.


Kweli, pahali pa kumuteketeza mufalme wa Asuria pamekwisha kutayarishwa muda murefu uliopita. Pahali penyewe ni shimo kubwa na pana. Kuna moto na kuni kwa uwingi. Yawe ataupulizia pumzi yake kama kijito cha kiberiti na kuuwasha.


Basi, malaika wa Yawe aliingia ndani ya kambi ya Waasuria na kuwaua watu elfu mia moja makumi nane na watano. Kesho yake, wakati watu walipoamuka, waliona yale maiti yote.


Bwana atawatakasa wanawake wa Sayuni toka uchafu wao na kusafisha damu iliyomwangika katika Yerusalema, kwa njia ya upepo wa hukumu na wa kuunguza.


Viatu vyote vya washambulizi katika vita na nguo zote zenye kujaa damu vitateketezwa kama kuni za kuwasha moto.


Utawala wake utastawi siku zote, amani ya ufalme wake haitakoma. Atakamata madaraka ya mufalme Daudi na kutawala juu ya ufalme wake; ataustawisha na kuuimarisha kwa kufuata sheria ya Mungu na kutenda kwa haki tangu sasa na hata milele. Yawe wa majeshi atafanya mambo hayo.


Siku zinakuja ambapo nitaotesha kichipukizi cha haki toka kizazi cha Daudi. Huyo atatawala kama mufalme, atatenda kwa hekima naye ataimarisha sheria yangu na haki katika inchi.


Watasikia shindo la kwato za farasi, kelele za magari ya vita, na vishindo vya magurudumu yao. Wababa watawasahau watoto wao, mikono yao itakuwa imeregea sana.


Wanaporukaruka kwenye vilele vya milima, wananguruma kama magari yenye kukokotwa na farasi, wanavuma kama moto wa majani yenye kukauka. Wamejipanga kama kundi kubwa la waaskari tayari kabisa kufanya vita.


Kuhani ataviteketeza hivyo vyote juu ya mazabahu kama vile chakula Yawe anachotolewa kwa moto.


Kuhani ataviteketeza juu ya mazabahu kama chakula kinachotolewa kwa Yawe kwa moto kutoa harufu ya kumupendeza Mungu. Mafuta yote ni ya Yawe.


Yawe anasema hivi: Lakini wewe Betelehemu katika Efurata, wewe ni mudogo tu kati ya ukoo wa Yuda, lakini kwako kutanitokea mutawala atakayetawala juu ya Israeli. Asili yake ni ya zamani sana.


Sikia! Mulio wa fimbo, mashindo ya magurudumu, vishindo vya farasi na ngurumo za magari ya vita!


Yeye ndiye atakayelijenga hekalu la Yawe. Atapewa heshima ya kifalme na kuikaa kwenye kiti chake cha kifalme kuwatawala watu wake. Kuhani Mukubwa ataikaa karibu na kiti cha kifalme cha mutawala yule, nao wawili watafanya kazi pamoja kwa amani.


Mimi ninawabatiza kwa maji kwa kuonyesha kwamba mumegeuka toka zambi zenu. Lakini yule atakayekuja nyuma yangu atawabatiza kwa Roho Mutakatifu na kwa moto. Yeye ni mwenye uwezo kunipita, nami sistahili hata kumuvua viatu.


Nami nitafanya maajabu juu katika mbingu na vitambulisho chini katika dunia: kutakuwa damu, moto na moshi mwingi.


Kisha wakaona mufano wa ndimi za moto zikitokea, nazo zikasambaa na kushuka juu ya kila mumoja wao.


katikati ya ndimi za moto kwa kuazibu wale wanaokataa kumujua Mungu na wale wasiokubali Habari Njema ya Bwana wetu Yesu.


Malaika wa Yawe akamujibu: “Kwa nini unataka kujua jina langu? Ni la ajabu.”


Saulo alipokuwa angali anaongea na kuhani, fujo katika kambi ya Wafilistini iliongezeka zaidi na zaidi. Kwa hiyo Saulo akamwambia kuhani: “Acha. Usililete tena Sanduku la Agano.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ