Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 9:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Wewe, ee Mungu, umeongoza taifa, umezidisha furaha yake. Watu wanafurahi mbele yako wana furaha kama kwa wakati wa mavuno, kama vile wanaogawanya vitu walivyonyanganya wanavyofurahi.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 9:2
22 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

mbele ya kwenda kule ambako sitarudi, kule kwenye inchi ya huzuni na giza kubwa;


Wengine waliishi katika giza na ukiwa, wafungwa katika mateso na minyororo,


Aliwatoa katika giza na ukiwa, na minyororo yao akaivunjavunja.


Hata nikipita katika bonde la giza kubwa, sitaogopa hatari yoyote, maana wewe, ee Yawe, ni pamoja nami; gongo lako na fimbo yako vinanipa moyo.


Lakini mimi umenijalia furaha kubwa ndani ya moyo, kuliko ya hao wanaokuwa na divai na ngano kwa wingi.


Nani kati yenu anayemwogopa Yawe? Nani anayetii maneno ya mutumishi wake? Kama kuna mutu anayetembea katika giza bila taa, amutumainie Yawe, na kumutegemea Mungu wake.


Hautahitaji tena jua kukuangazia muchana, wala mwezi kukuangazia usiku; maana mimi Yawe ni mwangaza wako milele; mimi Mungu wako nitakuwa utukufu wako.


Watu waliotembea katika giza wameona mwangaza mukubwa. Watu walioishi katika inchi ya giza kubwa, sasa mwangaza umewaangazia.


Huyo aliyezifanya nyota zinazoitwa Kilimia na Orioni, ambaye analigeuza giza nene kuwa muchana, na muchana kuwa usiku; yeye anayekusanya maji ya bahari na kuyamwanga juu ya inchi kavu, Yawe ndilo jina lake.


Watu hao wanaokaa katika giza, mwangaza umewatokea! Hao wanaoishi katika inchi yenye giza nzito sana ya lufu, wameona mwangaza mukubwa.”


Ndio utakaowaangazia mataifa, na kuleta utukufu kwa watu wako Waisraeli.”


Yesu akawaambia: “Mwangaza ungali kati yenu kwa muda kidogo. Mutembee wakati mungali na mwangaza, kusudi giza lisiwafunike, kwa sababu anayetembea katika giza hajui pahali anapokwenda.


Mimi nimekuja katika dunia kama mwangaza, kusudi mutu yeyote anayeniamini asikae katika giza.


Yesu akawaambia watu tena: “Mimi ni mwangaza wa dunia. Yeye anayenifuata hatatembea katika giza hata kidogo, lakini atakuwa na mwangaza wa uzima.”


Zamani muliishi katika giza, lakini sasa, kwa kuungana kwenu na Bwana, munaishi katika mwangaza. Muishi kama watoto wa mwangaza,


Lakini ninyi ni watu wa kizazi kilichochaguliwa na Mungu na wa ukuhani wa kifalme. Ninyi ni taifa takatifu na watu wa pekee wa Mungu. Mumechaguliwa kusudi mutangaze matendo makubwa ya yule aliyewaita kutoka katika giza na kuwaingiza kwenye mwangaza wake wa ajabu.


‘Bila shaka wanatafuta na kugawanyana vitu: binti mumoja au wawili kwa kila askari, nguo ya sufu ya rangi kwa ajili ya Sisera, nguo ya sufu iliyopindwa vizuri, na mikufu miwili yenye kufumwa kwa ajili ya shingo yangu!’


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ