Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 9:17 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

17 Uovu unawaka kama moto unaoteketeza michongoma na miiba; unawaka kama moto katika pori, na kutoa moshi muzito unaopanda juu katika anga.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 9:17
33 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wote wasiomwogopa Mungu hawatapata watoto, moto utateketeza mahema ya wanaokula kituliro.


Kusikuwe mutu wa kumutendea mema, au kuwatunza watoto wake wayatima!


Yeye hafurahii nguvu za farasi, wala hapendezwi na ushujaa wa waaskari;


Ole kwako wewe taifa lenye zambi, watu waliolemewa na uovu, kizazi cha watenda mabaya, watoto wanaoishi kwa udanganyifu! Ninyi mumemwacha Yawe, mumemuzarau Mutakatifu wa Israeli, mumerudi nyuma.


Wanakataa kusambisha wazaifu, wananyanganya watu wangu wamasikini haki yao. Wanateka wajane; wananyanganya wayatima mali yao.


Hakuna! Mutajikunja tu kati ya wafungwa na kuangamia pamoja na wanaouawa katika vita. Hata hivyo, hasira yake haijatulia, angali ananyoosha mukono wake kwa kuwaazibu.


Nilimutuma kuliazibu taifa ovu, nilimwamuru kuwaazibu watu niliowakasirikia, kuwanyanganya na kuteka vitu vyao, na kuwakanyaga chini kama matope katika njia.


Mishale yao itawaua vijana, hawatarehemu watoto, wala kuwahurumia watoto wachanga.


Lakini wewe hautaunganishwa nao katika mazishi, maana uliiharibu inchi yako, uliwaua watu wako. Wazao wa waovu wasahauliwe kabisa!


Watu wameichafua dunia maana wamezivunja sheria za Mungu, wamegeuka mbali na masharti yake, wamelivunja agano lake la milele.


Matawi ya miti yamekauka na kuvunjika; wanawake wanayaokota na kuyawasha moto. Watu hawa hawajaelewa kitu, kwa hiyo Mungu, Muumba wao, hatawahurumia, yeye aliyewafanya, hatawatendea mema.


Watu wa Yerusalema wamejikwaa, watu wa Yuda wameanguka, kwa sababu wanamupinga Yawe kwa maneno na matendo, wakizarau utukufu wake kati yao.


Mungu ni mwenye hekima na analeta maangamizi. Habadilishi masemi yake; lakini yuko tayari kuwaazibu watu waovu vilevile na wasaidizi wa watenda mabaya.


Wamisri ni wanadamu tu wala si miungu; farasi wao nao ni nyama tu, si roho. Yawe akiunyoosha mukono wake, taifa linalotoa musaada litajikwaa, na lile linalosaidiwa litaanguka; yote mawili yataangamia pamoja.


Mipango yenu yote ni kama maganda, na matokeo yake ni takataka tupu. Pumzi yangu itawaangamiza kama moto.


Watu watakuwa kama wamechomwa kuwa majivu, kama miiba iliyokatwa na kuteketezwa katika moto.


Hata vijana wataregea na kuchoka; kweli washujaa wataanguka kwa muchoko.


Kwa hiyo, kama vile moto unavyoteketeza nyasi, kama vile majani yanavyotoweka ndani ya moto, ndivyo mizizi yao itakavyooza, na maua yao yatakavyopeperushwa juu kama mavumbi. Maana wameacha sheria ya Yawe wa majeshi, wamezarau neno la yule Mutakatifu wa Israeli.


Kwa hiyo hasira ya Yawe iliwawakia watu wake, akaunyoosha mukono wake juu yao, akawaazibu. Milima ikatetemeka, maiti zao zikakuwa kama takataka katika barabara za muji. Hata hivyo, hasira yake haijatulia, angali ananyoosha mukono wake kwa kuwaazibu.


Maana kama vile kijana mwanaume anavyomwoa binti, ndivyo aliyekujenga atakavyokuwa mume wako. Kama bwana arusi anavyofurahi juu ya bibi arusi, ndivyo Mungu atakavyofurahi juu yako.


Nami nitaufurahia Yerusalema, nitawafurahia watu wangu. Sauti ya kilio haitasikilika tena, kilio cha taabu hakitakuwa tena.


Ingawa aliwaazibu watu, hawakumurudilia Yawe wa majeshi.


Kwa hiyo uwaache watoto wao wakufe kwa njaa, uwaache wakufe kwa vita. Wake zao wakuwe tasa na wajane. Waume zao wakufe kwa magonjwa makali na vijana wao wachinjwe kwa upanga katika vita.


Mukimbie huko na huko katika Yerusalema, mupeleleze na kujionea wenyewe, muchunguze katika masoko yake. Mukiona hata mutu mumoja anayefuata sheria, mutu anayetafuta ukweli, basi Yawe atausamehe Yerusalema.


Kama vile ninavyoishi, –ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe– nitawatawala kwa mukono wenye nguvu, kwa ukali na kuwamwangia kasirani yangu.


Niliwaletea ugonjwa mukali kama ule nilioupelekea Misri. Niliwaua vijana wenu katika vita, nikatwaa farasi wenu wa vita. Maiti zilijaa katika kambi zenu, harufu yake mbaya ikajaa katika pua zenu. Hata hivyo hamukunirudilia. –Ni ujumbe wa Yawe.–


Siku hiyo, wabinti wazuri na vijana wanaume watazimia kwa kiu.


Hakuna mutu mwaminifu kwa Mungu aliyebaki katika inchi, hakuna mutu yeyote mwenye usawa kati ya watu. Kila mumoja anavizia kumwanga damu; kila mumoja anamwinda mwenzake kusudi amunase.


Angalia jinsi gani uzuri na urembo wake unavyokuwa! Vijana wanaume na wanawake watastawi kwa wingi wa ngano na divai mupya.


Ninyi kikundi cha nyoka! Namna gani ninyi munaokuwa wabaya, munaweza kusema maneno mazuri? Kwa maana kinywa kinasema maneno yanayojaa ndani ya moyo.


Na asubui munapoona kwamba mawingu ni meusi munasema kwamba mvua itanyesha. Munajua kutambua hali ya mawingu, lakini hamuwezi kujua vitambulisho vya nyakati hizi.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ