Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 9:13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

13 Yawe atakata katika Israeli kichwa na mukia, tawi la mingazi na nyasi, kwa muda wa siku moja tu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 9:13
24 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wakati alipokuwa katika taabu zaidi, mufalme huyu Ahazi alizidi kumwasi Yawe.


Waovu wanapenda kukasirika; hawamwombi musaada anapowafunga.


Niwapige wapi tena, ninyi munaoendelea kuasi? Kichwa chote kinajaa vidonda, na moyo unaumia kabisa!


Hakuna mutu yeyote katika inchi ya Misri, mutawala au wanainchi, wakubwa au watu wadogo, anayeweza kufanya jambo lolote la maana.


Ee Yawe umeinua mukono kwa kuwaazibu, lakini hawauoni. Uwaonyeshe namna unavyowapenda watu wako nao watapata haya. Moto unaowatayarishia waadui zako, uwateketeze!


Ole kwao wale wanaokwenda Misri kuomba musaada! Wanategemea farasi, wanategemea wingi wa magari ya vita na nguvu za waaskari wao wapanda-farasi. Lakini hawamutegemei Mutakatifu wa Israeli, wala hawamwombi Yawe shauri!


Niliwakasirikia kwa sababu ya uovu na tamaa zao; niliwaazibu, nikauficha uso wangu na kukasirika. Lakini wao waliendelea kufuata njia zao wenyewe.


Wakati ule, Bwana atalipa wembe kutoka ngambo ya muto Furati, ni kusema mufalme wa Asuria. Atawanyoa vichwa vyenu, miili yenu na ndevu zenu vilevile.


Nimepepeta watu wangu kwa kuwasambaza sawa maganda, toka katika kila muji wa inchi yao. Nimewaangamiza kwa kuwaua watoto wao, lakini hawakuacha mwenendo wao.


Maana, mimi ninajua mupango ninaokuwa nao juu yenu. –Ni ujumbe wa Yawe.– Nayo mipango yangu ni ya kuwatendea mema wala si mabaya, kusudi mupate kuwa na tumaini katika siku zinazokuja.


Ee Yawe, wewe unatafuta uaminifu siku zote. Umewatwanga, lakini hawakuona uchungu; umewateketeza, lakini walikataa maonyo. Wamevifanya vichwa vyao kuwa vigumu kuliko jiwe; wamekataa kabisa kurudi kwako.


Wewe mwanadamu! Uwaambie Waisraeli kwamba inchi yao ni kama inchi ambayo haijanyeshewa, imenyauka kwa sababu ya kasirani yangu ikakuwa kama udongo bila maji.


Ewe Yerusalema, matendo yako machafu yamekuchafua. Ingawa nilijaribu kukutakasa, mwenyewe ulibaki muchafu. Basi, hautatakasika tena mpaka nitakapotuliza hasira yangu juu yako.


Umetuazibu kama ilivyoandikwa katika Sheria ya Musa, lakini mpaka sasa, ee Yawe, Mungu wetu, hatukuomba musamaha wako kwa kuziacha zambi zetu na kutambua uaminifu wako.


Nitarudi mahali pangu na kujitenga nao mpaka watambue kosa lao na kunirudilia. Taabu zao zitawafundisha wanitafute.


Kiburi cha Waisraeli kinawashuhudia wao wenyewe, hawanirudilii mimi Yawe, Mungu wao; wala hawanitafuti kwa ajili ya matukio hayo yote.


Wanaigeukia miungu ya bure, wako kama upinde ulioregea. Waongozi wao watakufa kwa upanga, kwa sababu ya maneno yao ya kiburi. Kwa hiyo, watazarauliwa katika inchi ya Misri.


Niliwaletea ugonjwa mukali kama ule nilioupelekea Misri. Niliwaua vijana wenu katika vita, nikatwaa farasi wenu wa vita. Maiti zilijaa katika kambi zenu, harufu yake mbaya ikajaa katika pua zenu. Hata hivyo hamukunirudilia. –Ni ujumbe wa Yawe.–


Mimi niliwanyima chochote cha kutafuna, nikasababisha ukosefu wa chakula popote. Hata hivyo hamukunirudilia. –Ni ujumbe wa Yawe.–


Nitawaangamiza wote walioniacha mimi Yawe, wote walioacha kunitafuta na kuniuliza shauri.


Kisha kutoka humohumo katika inchi mutamutafuta Yawe, Mungu wenu, nanyi mutamupata kama mukimutafuta kwa moyo wote na roho yote.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ