Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 8:18 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

18 Mimi pamoja na watoto Yawe alionipa ni kitambulisho na mufano katika Israeli kwa jina la Yawe wa majeshi anayekaa kwenye mulima Sayuni.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 8:18
27 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Esau alipoinua macho na kuwaona wale wamama na watoto, akauliza: “Ni wa nani hawa unaokuwa nao?” Yakobo akamujibu: “Hawa ni watoto ambao Mungu, kwa neema yake, amenijalia mimi mutumishi wako.”


Daudi akasema: “Yawe, Mungu wa Israeli, amewapa watu wake amani, naye ataishi Yerusalema kwa milele.


Wenye kiburi wote katika dunia watamwabudu; wote ambao ni wa kufa watainama mbele yake, wote ambao hawawezi kudumisha uzima wao.


Kwa wengi nimekuwa mushangao, lakini wewe ni kimbilio langu lenye nguvu.


Wanaojua jina lako, wanakutegemea, kwa maana wewe, ee Yawe, hauwatupi wanaokutafuta.


Mumwimbie sifa Yawe anayekaa Sayuni! Muyatangazie mataifa mambo aliyotenda!


Mupige vigelegele na kuimba kwa furaha, enyi wakaaji wa Sayuni, maana Mutakatifu wa Israeli ni makubwa kati yenu.


Basi watapewa jibu gani wajumbe wa taifa hilo? Wataambiwa: Yawe ameijenga imara Sayuni, na wamasikini kati ya watu wake watakimbilia kule.


Yawe akasema: Mutumishi wangu Isaya amekuwa akitembea uchi na bila viatu kwa muda wa miaka mitatu sasa, kama kitambulisho juu ya inchi za Misri na Kushi.


Kisha mwezi utafezeheka, nalo jua litapata haya ya kuangaza, maana Yawe wa majeshi atatawala kule Yerusalema katika mulima Sayuni; ataonyesha wazee wa watu wake utukufu wake.


Yawe alipenda kumuponda kwa mateso. Alitoa uzima wake kwa ajili ya kuondoa zambi. Mutumishi wa Mungu atakuwa na wazao; ataishi maisha marefu. Yeye ndiye atakayetimiza mupango wa Yawe.


Maana, mbele mutoto huyo hajajua kukataa mabaya na kuchagua mema, inchi za wafalme hao wawili unaowaogopa zitakuwa ukiwa.


Yawe akamwambia Isaya: Uende pamoja na mwana wako anayeitwa Watakaobaki-Watarudi, kukutana na mufalme Ahazi. Utamukuta katika barabara pahali wafuaji wa nguo wanapofanyia kazi, mwisho wa mufereji unaoleta maji kutoka kwenye birika la juu.


Nikalala na muke wangu ambaye vilevile ni nabii, akapata mimba, akazaa mutoto mwanaume. Yawe akaniambia: Umupe mutoto huyo jina “Teka-haraka-nyanganya-upesi.”


Nitawaazibu hapahapa mupate kujua kwamba maneno ya hasara niliyosema juu yenu yatatimia. –Ni ujumbe wa Yawe.– Na hiki kitakuwa kitambulisho chake:


Wakiwa wanakuona, ujibebeshe muzigo wako kwenye mabega na kuondoka wakati wa giza. Funika uso wako usiweze kuona unakwenda wapi. Ndivyo ninavyokufanya kuwa kitambulisho kwa Waisraeli.


Nitapingana naye. Nitamufanya kuwa kitambulisho na mufano; nitamwondoa kabisa kutoka taifa langu. Halafu mutatambua kwamba mimi ni Yawe.


Nawe utwae bamba la chuma. Ulisimamishe likuwe kama ukuta wa chuma kati yako na muji. Kisha utaelekezea muji huo uso wako nao utashambuliwa na utaushambulia. Hiki kitakuwa kitambulisho kwa taifa la Waisraeli.


Sasa sikiliza kwa uangalifu, ewe Yoshua, Kuhani Mukubwa; musikilize vilevile enyi makuhani wenzake munaokuwa pamoja naye, ninyi munaokuwa kitambulisho cha wakati muzuri unaokuja: Nitamuleta mutumishi wangu anayeitwa Tawi.


Yawe wa majeshi anasema hivi: Nitaurudilia Sayuni na kufanya makao yangu katika Yerusalema. Muji Yerusalema utaitwa “Muji Mwaminifu”, na mulima wa Yawe wa majeshi utaitwa “Mulima Mutakatifu”.


Na wote waliosikia habari ile waliyoieleza wakashangaa.


Simeoni akawabariki na kumwambia Maria, mama yake: “Mutoto huyu amezaliwa kwa sababu ya kuwaangusha na kuwasimamisha watu wengi katika Israeli. Naye atakuwa kitambulisho kutoka kwa Mungu watu watakachokipinga,


Lakini hizo zitakuwa ushuhuda wa hukumu ya Yawe kwenu na wazao wenu milele.


Kwa ngambo moja mulitukanwa na kuteswa waziwazi mbele ya watu. Na kwa ngambo ingine mulishirikiana na wale waliotendewa vibaya.


Lakini ninyi mumefikia kwenye mulima Sayuni na kwenye muji wa Mungu Mwenye Uzima, ndio muji Yerusalema wa mbinguni, kunakokuwa maelfu na maelfu ya wamalaika.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ