Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 8:17 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

17 Nitamungojea Yawe ambaye amejificha mbali na wazao wa Yakobo; nitamutumainia.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 8:17
39 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mbona unageuza uso wako mbali nami? Kwa nini unanitendea kama adui yako?


Mutu akikufa anaweza kuishi tena? Siku zangu zote za kazi ningekungoja mpaka wakati wa kufunguliwa ufike.


Atakujibu namna gani wakati wewe unasema kwamba haumwoni na kwamba maneno yako iko mbele yake na wewe unamungojea!


Ninamutumainia Yawe kwa moyo wangu wote. Ninaaminia sana neno lake.


Umutegemee Yawe! Ujitie moyo, ukuwe hodari! Umutegemee Yawe!


Mioyo yetu inamutumainia Yawe. Yeye ni musaidizi wetu na ngao yetu.


Umutumainie Yawe na kushika njia yake, naye atakuinua uirizi inchi, na kuwaona waovu wakiongolewa.


Kweli, kila mutu anapita kama kivuli; masumbuko yake yote ni bure tu; anakusanya mali, hajui atakayeipata!


Munapoinua mikono yenu kwa kuomba, nitauficha uso wangu nisiwaone. Hata mukiomba sana sitawasikia, maana mikono yenu imejaa damu.


Siku ile, watu wote watasema: Huyu ndiye Mungu wetu! Tumemungojea atuokoe. Huyu ndiye Yawe tuliyemutazamia. Mukuje tufurahi na kushangilia kwa sababu ametuokoa.


Katika njia ya maamuzi yako tunakungojea ee Yawe; tamaa yetu ni kulikumbuka jina lako.


Hata hivyo, Yawe anangoja kuwasamehe, atasimama na kuwaonea huruma. Yawe ni Mungu wa haki. Heri wote wale wanaomutumainia.


Ee Yawe, utuonee huruma, kwako tumeliweka tumaini letu. Ukuwe kikingio chetu kila siku, mwokozi wetu wakati wa taabu.


Kweli wewe ni Mungu mwenye kufichama, Mungu wa Israeli, Mungu mwokozi.


Nani kati yenu anayemwogopa Yawe? Nani anayetii maneno ya mutumishi wake? Kama kuna mutu anayetembea katika giza bila taa, amutumainie Yawe, na kumutegemea Mungu wake.


Kwa hasira nyingi nilikuficha uso wangu kwa muda kidogo, lakini kwa wema wa milele nitakuonea huruma. Ni Yawe Mukombozi wako anayesema hivyo.


Niliwakasirikia kwa sababu ya uovu na tamaa zao; niliwaazibu, nikauficha uso wangu na kukasirika. Lakini wao waliendelea kufuata njia zao wenyewe.


Zambi zenu ndizo zinazowatenga na Mungu wenu, zambi zenu zimemufanya ajifiche mbali nanyi hata asiweze kuwasikiliza ninyi.


Wewe unakuja kuwasaidia wanaotenda haki kwa furaha, wanaokukumbuka na kufuata njia zako. Ulitukasirikia tulipokuwa wenye zambi; sisi tumeasi kwa muda murefu.


Hakuna hata mumoja anayekuja kukuomba; hakuna anayejishugulisha kukutafuta. Wewe unauficha uso wako mbali nasi, umetuacha tufungwe na maovu yetu.


Hata hivyo, ee Yawe, wewe ni Baba yetu. Sisi ni kama udongo, wewe ni mufinyanzi. Sisi wote ni kazi ya mikono yako.


Watu watajaribu kupigana na Wakaldea lakini hiyo itakuwa bure, maana mifereji itajaa maiti za watu ambao nitawaua kwa hasira na kasirani yangu. Kwa vile wamefanya uovu huo wote, mimi nitauacha muji huu.


Wakati unakuja ambapo mutamulilia Yawe, lakini yeye hatawajibu. Atauficha uso wake wakati huo, kwa sababu mumetenda mambo maovu.


Lakini mimi ninamutumainia Yawe, ninamutazamia Mungu mwenye kuniokoa; Mungu wangu atanisikiliza.


Maono haya yanangoja wakati uliopangwa; ni maono ya ukweli juu ya mwisho. Kama yanaonekana kuchelewa, uyangojee; hakika yatafika, wala hayatachelewa.


Basi, akafika saa ile ile, akaanza kumushukuru Mungu. Naye akaeleza habari za mutoto huyo kwa watu wote waliokuwa wakingojea jinsi Mungu atakavyokomboa Yerusalema.


Kisha akawaelezea maneno yaliyoandikwa juu yake katika Maandiko Matakatifu yote, akianza toka vitabu vya Musa na kuendelea katika vitabu vya manabii wote.


Akasema hivi: Nitawaficha uso wangu nione mwisho wao utakuwa namna gani. Maana wao ni kizazi kipotovu, watoto wasiokuwa na uaminifu wowote.


na kungojea Mwana wake Yesu kutoka mbinguni. Ni yule Mungu aliyemufufua, naye ndiye anayetuokoa toka kasirani ya hukumu ya Mungu inayokuja.


Bwana aongoze mafikiri yenu katika upendo wa Mungu na katika uvumilivu tunaopewa na Kristo.


Tena anasema: “Nitamutumainia Mungu.” Na tena anasema: “Mimi ni hapa pamoja na watoto Mungu alionipatia.”


Hivi vilevile Kristo naye alijitoa kufa mara moja kusudi aondoe zambi za watu wengi. Naye atarudi tena, si kwa ajili ya kuondoa zambi, lakini kwa kuwaokoa wale wanaomungojea.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ