Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 8:14 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

14 Mimi nitakuwa kimbilio. Nitakuwa vilevile kama jiwe la kujikwaa, jiwe kubwa la kuziangusha falme za Israeli na Yuda. Nitakuwa mutego wa kuwatega na kuwanasa wakaaji wa Yerusalema.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 8:14
24 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Atawanyeshea waovu makaa ya moto na kiberiti; upepo mukali utakuwa ndio azabu yao.


Ee Yawe, unilinde na makucha ya wabaya; unikinge na watesaji wakali ambao wamepanga kuniangusha.


Walinipa sumu ndani ya chakula, na nilipokuwa na kiu wakanipa divai inayochacha.


Jina la Yawe ni munara imara; mwenye haki anaukimbilia na kuwa salama.


Maana wewe umekuwa kimbilio kwa wazaifu, pango kwa wakosefu katika taabu zao. Wewe ni kimbilio wakati wa zoruba, kivuli wakati wa joto kali. Kweli pigo la watu wakali ni kali kama zoruba inayopiga ukuta;


Mukuje watu wangu, muingie ndani ya nyumba zenu, mujifungie humo ndani. Mujifiche kwa muda mufupi, mpaka kasirani ya Yawe ipite.


Basi, Bwana wetu Yawe anasema hivi: Ninaweka katika Sayuni jiwe la musingi, jiwe ambalo limeimarishwa. Jiwe la pembe, la bei kali, jiwe ambalo ni la musingi imara; jiwe linalokuwa na maandiko haya: Anayeamini hataanguka.


Utukufu wake utakuwa kwao kivuli kwa kuwakinga na joto la muchana; na kimbilio na kikingio chao wakati wa zoruba na mvua.


Kama vipofu tunapapasapapasa ukuta; tunasitasita kama watu wasiokuwa na macho. Tunajikwaa muchana kati, sawa vile ni usiku; kati ya wenye afya, sisi ni kama wafu.


Maana, mbele mutoto huyo hajajua kukataa mabaya na kuchagua mema, inchi za wafalme hao wawili unaowaogopa zitakuwa ukiwa.


Kwa hiyo Yawe anasema hivi: Nitawawekea watu hawa vikwazo, ambavyo vitawaangusha chini. Wababa na wana wataangamia, na jirani na rafiki vilevile.


Lakini, uwaambie hao wanaokuwa katika uhamisho kwamba Bwana wao Yawe anasema hivi: Ingawa nimewapeleka mbali kati ya mataifa na kuwasambaza katika inchi zingine, hata hivyo, mimi nipo pamoja nao huko wanakokuwa, kama vile hekalu kwao.


Tena, kama mutu wa haki akigeuka katika haki yake na kutenda uovu, nami nikimwekea kikwazo, mutu huyo atakufa. Kwa vile haukumwonya, atakufa kwa sababu ya zambi yake, nayo matendo yake ya haki hayatakumbukwa. Lakini wewe utabeba lazima ya damu yake.


Na kwa hiyo akakuwa kikwazo kwao. Lakini Yesu akawaambia: “Nabii hakosewi heshima fasi zote, isipokuwa tu katika muji wake na katika jamaa yake.”


Anayeanguka juu ya jiwe hili atavunjikavunjika, na yule litakayemwangukia, atapondekana.]”


Simeoni akawabariki na kumwambia Maria, mama yake: “Mutoto huyu amezaliwa kwa sababu ya kuwaangusha na kuwasimamisha watu wengi katika Israeli. Naye atakuwa kitambulisho kutoka kwa Mungu watu watakachokipinga,


sawa mutego. Kwa maana Siku ile itawafikia watu wote wa dunia.


Ni nani anayeweza kumupa Mungu kitu kwanza, kusudi naye apate kumurudishia?”


Basi, Yoshua pamoja na jeshi lake lote na mashujaa wakaondoka Gilgali.


Tena imeandikwa kwamba: “Jiwe lile ni la kukwalisha watu, nalo ni la kuwaangusha.” Wamejikwaa kwa sababu hawakuamini neno la Mungu, na hivi ndivyo walivyopanga kwa ajili yao tangu mwanzo.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ