Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 8:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Yawe aliniambia hivi: Twaa ubao mukubwa, uandike juu yake maneno yanayosomeka waziwazi: “Teka haraka. Nyanganya Upesi.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 8:1
11 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mungu aliniambia: Sasa andika jambo hili mbele yao, juu ya kibao na katika kitabu, likuwe ushuhuda wa milele:


Nitalinda agizo hilo na kuchunga mafundisho hayo kati ya wafuasi wangu.


Nikalala na muke wangu ambaye vilevile ni nabii, akapata mimba, akazaa mutoto mwanaume. Yawe akaniambia: Umupe mutoto huyo jina “Teka-haraka-nyanganya-upesi.”


Yawe, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Andika katika kitabu maneno yote ninayokuambia.


Twaa kizingo cha kitabu uandike humo maneno yote niliyokuambia juu ya Israeli, juu ya Yuda na mataifa yote, tangu siku nilipoanza kusema nawe, wakati Yosia alipokuwa mufalme mpaka leo.


Twaa kitabu kingine, uandike maneno yote yaliyokuwa katika kile cha kwanza ambacho Yoyakimu, mufalme wa Yuda, amechoma kwa moto.


Kisha, Yeremia alitwaa kitabu kingine, akamupa katibu Baruku mwana wa Neria, ambaye aliandika humo maneno yote aliyoambiwa na Yeremia ambayo yalikuwa katika kile kitabu cha mbele ambacho Yoyakimu, mufalme wa Yuda, alichoma kwa moto. Maneno mengine ya namna hiyo yaliongezwa.


Hapa inafaa kuwa na hekima. Yule anayekuwa na akili afafanue hesabu ya tarakimu zinazolingana na jina la yule nyama, kwa maana tarakimu ile ni ya mutu fulani. Nayo ni mia sita makumi sita na sita.


Malaika akapima vilevile ukuta; ulikuwa yapata metre makumi sita kufuatana na kipimo cha kawaida cha wanadamu ambacho yule malaika alichotumia.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ