Nikalala na muke wangu ambaye vilevile ni nabii, akapata mimba, akazaa mutoto mwanaume. Yawe akaniambia: Umupe mutoto huyo jina “Teka-haraka-nyanganya-upesi.”
Twaa kizingo cha kitabu uandike humo maneno yote niliyokuambia juu ya Israeli, juu ya Yuda na mataifa yote, tangu siku nilipoanza kusema nawe, wakati Yosia alipokuwa mufalme mpaka leo.
Kisha, Yeremia alitwaa kitabu kingine, akamupa katibu Baruku mwana wa Neria, ambaye aliandika humo maneno yote aliyoambiwa na Yeremia ambayo yalikuwa katika kile kitabu cha mbele ambacho Yoyakimu, mufalme wa Yuda, alichoma kwa moto. Maneno mengine ya namna hiyo yaliongezwa.
Hapa inafaa kuwa na hekima. Yule anayekuwa na akili afafanue hesabu ya tarakimu zinazolingana na jina la yule nyama, kwa maana tarakimu ile ni ya mutu fulani. Nayo ni mia sita makumi sita na sita.