Isaya 7:20 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
20 Wakati ule, Bwana atalipa wembe kutoka ngambo ya muto Furati, ni kusema mufalme wa Asuria. Atawanyoa vichwa vyenu, miili yenu na ndevu zenu vilevile.
Shoka litaweza kujisifu mbele ya yule anayelitumia? Musumeno unaweza kujivuna mbele ya mwenye kukata nao? Ni kama kwamba vile fimbo ingeweza kumwinua anayeishika, au gongo kumwinua mwenye kuitumia!
Yawe atakausha guba ya bahari ya Misri, kwa pumzi yake inayochoma atakausha muto Furati, nao utagawanyika katika vijito saba, watu wavuke humo miguu mikavu.
Katika mwaka wa kumi na ine wa utawala wa mufalme Hezekia, mufalme Saniharibu wa Asuria aliishambulia miji yote yenye kuta ya inchi ya Yuda na kuinyanganya.
Wewe mwanadamu! Nebukadneza, mufalme wa Babeli, aliwalazimisha waaskari wake kufanya kazi ngumu ya kuishambulia Tiro. Vichwa vyote vya waaskari wake vilipata upaa na mabega yote yalichubuka. Lakini yeye, wala waaskari wake, hawakupata chochote kutokana na kazi hiyo aliyoifanya juu ya Tiro.