Isaya 7:18 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
18 Wakati huo, Yawe atawapigia muunzi watu wa Misri wakuje kama mainzi toka vijito vya mito Nili; na watu wa Asuria wakuje kama nyuki kutoka inchi yao.
Halafu mufalme wa Misri akawaita Musa na Haruni, akawaambia: “Munaweza kwenda kutoa sadaka kwa Mungu wenu, lakini ikuwe humuhumu katika inchi ya Misri.”
Ole kwao wale wanaokwenda Misri kuomba musaada! Wanategemea farasi, wanategemea wingi wa magari ya vita na nguvu za waaskari wao wapanda-farasi. Lakini hawamutegemei Mutakatifu wa Israeli, wala hawamwombi Yawe shauri!
Yawe atakuletea wewe pamoja na watu wako na jamaa yote ya kifalme siku za taabu kuliko zile zote zilizotokea tangu wakati watu wa Efuraimu walipojitenga na watu wa Yuda; ni kusema, atawaletea ninyi mufalme wa Asuria.
Hapo, Waamori waliokuwa wanaishi katika eneo hilo la milima wakateremuka kuwashambulia na kama vile nyuki wanavyofanya wakawapiga huko Seiri mpaka Horma.