Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 7:14 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

14 Basi, Bwana mwenyewe atawapa kitambulisho: bikira atapata mimba, atazaa mutoto mwanaume na kumwita jina lake “Emanueli – Mungu Yuko Pamoja Nasi”.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 7:14
29 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kisha huyo malaika wa Yawe akamwambia: “Wewe una mimba na utazaa mutoto mwanaume; utamwita Isimaeli, maana Yawe ameyaona mateso yako.


Lea akapata mimba, akazaa mutoto mwanaume, akamwita Rubeni, akisema: “Yawe ameona mateso yangu; bila shaka sasa mume wangu atanipenda.”


Nitaweka uadui kati yako na yule mwanamuke, kati ya uzao wako na uzao wake. Yeye ataponda kichwa chako, nawe utamwuma kisigino chake.”


Rakeli akasema: “Mungu amenitendea sawa, amesikia kilio changu na kunipa mutoto mwanaume.” Akamwita mutoto yule Dani.


Halafu Rakeli akasema: “Nimepigana mapigano makubwa na dada yangu, nami nimeshinda.” Kwa hiyo akamwita mutoto yule Nafutali.


Adamu akalala tena na Eva muke wake, naye akazaa mutoto mwanaume, akamwita Seti akisema: “Mungu amenijalia mutoto pahali pa Abeli aliyeuawa na Kaina.”


Mutu huyo akaonyesha kitambulisho siku ileile, akasema: “Hiki ndicho kitambulisho Yawe alichosema: ‘Mazabahu hii itabomoka, na majivu yanayokuwa juu yake yatamwangika.’ ”


Yawe wa majeshi yuko pamoja nasi, Mungu wa Yakobo ni kimbilio letu.


Isaya akamujibu: Hiki kitakuwa kitambulisho kwako kutoka kwa Yawe kwamba Yawe atafanya kama alivyoahidi.


Mushauriane pamoja lakini itakuwa bure; mufanye mipango lakini haitawezekana, maana Mungu Yuko Pamoja Nasi.


Utaingia ndani ya inchi ya Yuda kwa nguvu na kufurika na kupanda mpaka kwenye shingo. Utaenea juu ya inchi yako yote, ee Emanueli!


Utawala wake utastawi siku zote, amani ya ufalme wake haitakoma. Atakamata madaraka ya mufalme Daudi na kutawala juu ya ufalme wake; ataustawisha na kuuimarisha kwa kufuata sheria ya Mungu na kutenda kwa haki tangu sasa na hata milele. Yawe wa majeshi atafanya mambo hayo.


Katika siku za utawala wake, inchi ya Yuda itaokolewa na inchi ya Israeli itakuwa katika usalama. Naye ataitwa kwa jina la Yawe Ni Haki Yetu.


Utasitasita mpaka wakati gani, ewe binti usiyekuwa mwaminifu? Maana, mimi nimefanya kitu kipya katika dunia; mwanamuke anamulinda mwanaume.


Nitawaazibu hapahapa mupate kujua kwamba maneno ya hasara niliyosema juu yenu yatatimia. –Ni ujumbe wa Yawe.– Na hiki kitakuwa kitambulisho chake:


Hivyo Mungu atawaachilia watu wake kwa waadui, mpaka yule mwanamuke mwenye kuwa na mimba atakapozaa. Kisha wandugu zake waliobakia, watarudi na kuungana na Waisraeli wenzao.


“Angalia bikira atapata mimba, atazaa mutoto mwanaume, naye ataitwa Emanueli,” (maana yake “Mungu yuko pamoja nasi”).


Utapata mimba, utazaa mutoto mwanaume, na utamwita jina lake Yesu.


Malaika akamujibu: “Roho Mutakatifu atakufikia, na uwezo wa Mungu Mukubwa utakufunika kama vile kivuli. Kwa sababu hii mutoto yule atakayezaliwa ataitwa Mutakatifu na Mwana wa Mungu.


Na hiki ndicho kitambulisho kwenu: mutamukuta mutoto muchanga amefunikwa nguo za kitoto, naye amelalishwa katika sanduku ya kukulishia nyama.”


Daudi anamwita Kristo ‘Bwana’; namna gani basi Kristo anaweza kuwa Mwana wake?”


Neno alifanywa kuwa mutu, naye akaishi kati yetu, akijaa neema na ukweli. Tuliona utukufu wake, utukufu ule Mwana wa pekee aliopewa na Baba.


Wao ni wazao wa babu zetu, na Kristo alizaliwa kimwili katika kizazi chao. Yeye ndiye mukubwa kupita wote na Mungu anayesifiwa kwa milele! Amina.


Hakika siri ya ibada yetu ni kubwa: Yeye alitokea kwa mufano wa mutu, alishuhudiwa na Roho Mutakatifu kuwa mwenye haki. Alionekana na wamalaika. Alitangazwa katikati ya mataifa. Aliaminiwa popote katika dunia. Na alinyanyuliwa mbinguni katika utukufu.


Gideoni akamwambia Mungu: “Ikiwa utaikomboa Israeli kwa mukono wangu kama ulivyosema,


Hivyo Hana akapata mimba, akazaa mutoto wa kiume. Hana akamwita mutoto huyo Samweli, maana alisema: “Nimemwomba kwa Yawe.”


Naye akamwita mutoto wake Ikabodi, maana alisema: “Utukufu wa Mungu umeondolewa kwa Waisraeli”, akiwa na maana kwamba Sanduku la Agano lilikuwa limetekwa, tena baba mukwe wake na mume wake, wote walikufa.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ