Musiniletee tena matoleo yenu yasiyokuwa na maana; ninachukizwa na sadaka yenu ya ubani. Muache kufanya sikukuu za mwandamo wa mwezi, Sabato na mikutano ya ibada; sikubali ibada zilizochanganyika na maovu.
Siku ile wazao wa Yakobo watakaobaki, ni kusema Waisraeli watakaopona hawatalitegemea tena taifa lililowaazibu, lakini watamutegemea kabisa Yawe, Mutakatifu wa Israeli.
Waefuraimu wanaendelea kutenda zambi, wanajitengenezea sanamu za feza yenye kuyeyushwa, sanamu zinazotengenezwa kwa ufundi wao, zote zikiwa kazi ya wafundi. Wanasema: Muzitambikie! Wanaume wanabusu sanamu ya mwana-ngombe!