Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 7:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Katika siku za utawala wa Ahazi mwana wa Yotamu na mujukuu wa Uzia, wa inchi ya Yuda, Resini, mufalme wa Aramu, na Peka mwana wa Remalia, mufalme wa Israeli, walienda kuushambulia Yerusalema, lakini hawakuweza kuunyanganya.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 7:1
15 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Peka mwana wa Remalia, ambaye alikuwa mukubwa wa waaskari wa Pekahia, alishirikiana na watu wengine makumi tano kutoka Gileadi, akamwua Pekahia katika chumba cha ndani cha nyumba ya mufalme kule Samaria na kuwa mufalme kwa pahali pake.


Katika mwaka wa makumi tano na mbili wa utawala wa mufalme Azaria wa Yuda, Peka mwana wa Remalia akaanza kutawala akiwa kule Samaria kwa muda wa miaka makumi mbili.


Wakati wa utawala wa Yotamu, Yawe akaanza kutuma mufalme Resini wa Aramu na mufalme Peka wa Israeli kwa kushambulia inchi ya Yuda.


Katika mwaka wa kumi na saba wa utawala wa Peka mwana wa Remalia, mufalme wa Israeli, Ahazi mwana wa Yotamu, mufalme wa Yuda, akaanza kutawala.


Kisha Resini mufalme wa Aramu na Peka mwana wa Remalia mufalme wa Israeli walitokea kwa kupiga vita na Yerusalema, nao waliuzunguka, lakini hawakuweza kuuteka.


Haya ni maono Isaya mwana wa Amozi, aliyoyaona juu ya inchi ya Yuda na Yerusalema, katika nyakati za utawala wa wafalme hawa wa Yuda: Ahazi na Hezekia.


Kwa sababu watu hawa wameyakataa maji ya Siloa yanayotiririka polepole, wakatetemeka mbele ya mufalme Resini na mufalme Peka mwana wa Remalia,


Waasuria kwa upande wa mashariki, Wafilistini kwa upande wa magaribi, wamepanua vinywa vyao kwa kuimeza Israeli. Hata hivyo, hasira yake haijatulia, angali ananyoosha mukono wake kwa kuwaazibu.


Watu wa Edomu walifanya biashara nawe kwa sababu ya wingi wa vitu vyako. Kwa kupata vitu vyako walikupa akiki, vitambaa vya rangi nyekundu-nyeusi, vitambaa vilivyopindwa vizuri, kitani safi, matumbawe na yakuti.


Hili ni neno ya Yawe lililomufikia Hosea mwana wa Beri katika siku za utawala wa Uzia, Yotamu, Ahazi na Hezekia, wafalme wa Yuda, na Yeroboamu mwana wa Yoasi, mufalme wa Israeli.


Hili ni neno la Yawe lilomufikia Mika, wa muji wa Moreseti wakati Yotamu, Ahazi na Hezekia walipokuwa wafalme wa Yuda. Mika aliona mambo yote haya juu ya Samaria na Yerusalema.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ