Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 66:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Musikilize neno la Yawe, enyi munaotetemeka kwa sababu ya neno lake. Wandugu zenu ambao wanawachukia, na kuwafukuza kwa sababu yangu, wamesema hivi kwa kuwachekelea: Mungu aonyeshe utukufu wake, nasi tuwaone ninyi mukishinda! Lakini wao wenyewe ndio watakaopata haya!

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 66:5
32 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

“Umeona jinsi Ahabu alivyojinyenyekeza mbele yangu? Basi, kwa sababu amejinyenyekeza, sitaleta yale maangamizi atakapokuwa angali anaishi, lakini nyakati za utawala wa mwana wake nitaiangamiza jamaa ya Ahabu.”


Kisha Safanu, mwandishi akamwambia mufalme: “Kuhani Hilkia amenipa kitabu.” Naye Safanu akakisoma mbele ya mufalme.


kwa sababu umetubu na kunyenyekea mbele yangu, hata umepasua nguo yako na kulia uliposikia maneno yangu juu ya pahali hapa, na juu ya wakaaji wake, na umejinyenyekeza mbele yangu, nami vilevile nimekusikia. –Ni ujumbe wa Yawe.–


Halafu watu wote walioshikwa na hofu kwa sababu ya maneno Mungu wa Israeli aliyosema juu ya makosa ya wale waliorudi kutoka katika uhamisho wakaanza kukusanyika karibu nami nikiwa mwenye kufazaika mpaka magaribi, wakati wa kutoa sadaka.


Ninatetemeka kwa kukuogopa wewe; nimejaa hofu kwa sababu ya maamuzi yako.


Waadui zangu ni wazima, wana nguvu, ni wengi sana hao wanaonichukia bure.


Anayezarau mashauri anajiletea maangamizi, lakini anayetii amri atapewa zawadi.


Musinishangae kwa sababu mimi ni mweusi. Ni kwa sababu jua limenichoma. Wandugu zangu walinikasirikia, wakanifanya kuwa mutumishi katika mashamba ya mizabibu. Lakini sikuchunga shamba langu la mizabibu.


Ee Yawe umeinua mukono kwa kuwaazibu, lakini hawauoni. Uwaonyeshe namna unavyowapenda watu wako nao watapata haya. Moto unaowatayarishia waadui zako, uwateketeze!


Wanasema: Muache Yawe afanye haraka, tunataka kuona yale aliyosema atayafanya! Mutakatifu wa Israeli atimize basi kusudi lake kusudi tuone ana mipango gani!


Wewe ulikuwa umeachwa na kuchukiwa, hakuna aliyependa hata kupita ndani yako. Lakini sasa nitakufanya ukuwe na utukufu milele, utakuwa muji wa furaha kwa kizazi na kizazi.


Basi, mimi Yawe ninasema: Watumishi wangu watakula, lakini ninyi mutasikia njaa; watumishi wangu watakunywa, lakini ninyi mutasikia kiu; watumishi wangu watafurahi, lakini ninyi mutafezeheka.


Mimi mwenyewe nilivifanya vitu hivi vyote, na hivi vyote ni mali yangu. Lakini ninachojali mimi, ni mutu munyenyekevu na mwenye moyo wenye kuvunjika, mutu anayetetemeka anaposikia neno langu. –Ni ujumbe wa Yawe.


Waliposikia maneno hayo yote, waliangaliana kwa hofu. Wakamwambia Baruku: Tunapaswa kumwelezea mufalme maneno haya yote.


Watanifuata mimi Yawe ninayenguruma kama simba; nitakaponguruma watanifikia toka magaribi wakitetemeka.


Na watu wote watawachukia kwa ajili yangu. Lakini atakayevumilia mpaka mwisho ataokolewa.


Yesu aliposema vile, wapinzani wake wote wakafezeheka, lakini kundi lote la watu wote walifurahia matendo yote ya ajabu aliyoyatenda.


Watawatenga musiingie katika nyumba za kuabudia. Na kutakuwa wakati ambapo wote watakaowaua watazani kwamba wanamutumikia Mungu.


Wakamujibu: “Wewe, uko mwenye zambi kabisa tangu kuzaliwa kwako! Unataka kutufundisha?” Halafu wakamufukuza inje.


Kwa hivi mutatukuza jina la Bwana wetu Yesu, nanyi mutatukuzwa naye kwa neema ya Mungu wetu na ya Bwana Yesu Kristo.


Na hivi tutaishi tukingojea ule uheri tunaoutumainia, wakati utukufu wa Mungu wetu Mukubwa na Mwokozi wetu Yesu Kristo utakapotokea.


Hivi vilevile Kristo naye alijitoa kufa mara moja kusudi aondoe zambi za watu wengi. Naye atarudi tena, si kwa ajili ya kuondoa zambi, lakini kwa kuwaokoa wale wanaomungojea.


Basi wandugu zangu, musishangae kama watu wa dunia hii wakiwachukia ninyi.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ