Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 66:22 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

22 Kama vile mbingu mupya na dunia mupya nitakazoumba zitakavyodumu milele kwa uwezo wangu, ndivyo wazao wako na jina lako litakavyodumu. –Ni ujumbe wa Yawe.–

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 66:22
19 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wazao wako wangekuwa wengi kama muchanga, kama chembe za muchanga. Jina lao lisingalisahauliwa hata kidogo, wala halingalifutwa mbele yangu.


Nimeyaweka maneno yangu katika kinywa chako; nimekuficha katika kivuli cha mukono wangu. Mimi nilizitandaza mbingu, nikaiweka misingi ya dunia. Mimi ninawaambia, enyi watu wa Sayuni: Ninyi ni watu wangu.


Yawe alipenda kumuponda kwa mateso. Alitoa uzima wake kwa ajili ya kuondoa zambi. Mutumishi wa Mungu atakuwa na wazao; ataishi maisha marefu. Yeye ndiye atakayetimiza mupango wa Yawe.


nitamupatia nafasi ya ukumbusho na ya sifa katika nyumba yangu na kuta zangu, nafasi bora kuliko kuwa na wana na wabinti. Nitamupatia jina la kukumbukwa siku zote na ambalo halitafutwa hata kidogo.


Yawe anasema: Mimi ninafanya nanyi agano hili: Roho wangu anayekuwa juu yenu, maneno niliyoyaweka katika kinywa chenu, hayataondoka kwenu hata kidogo, wala kwa watoto na wajukuu wenu, tangu sasa na hata milele.


Mimi Yawe ninapenda watu wafuate sheria yangu; ninachukia unyanganyi na uovu. Nitawatunza watu wangu kwa uaminifu, nitafanya nao agano la milele.


Wazao wao watajulikana kati ya mataifa; watajulikana kati ya watu wengine. Kila mutu atakayewaona atakubali kwamba wao ni watu waliobarikiwa na Yawe.


Sasa, ninaumba mbingu mupya na dunia mupya. Mambo ya zamani hayatakumbukwa tena.


Hawatajenga nyumba na watu wengine wakae ndani yake, wala kulima chakula kikuliwe na watu wengine. Maana watu wangu niliowachagua wataishi maisha marefu kama miti; wachaguliwa wangu watafurahia matunda ya jasho lao.


Kazi zao hazitakuwa bure, wala hawatazaa watoto watakaopatwa na musiba; maana watakuwa waliobarikiwa na Yawe, wamebarikiwa wao pamoja na wazao wao.


Yawe anasema hivi: Kama munaweza kuvunja agano langu nililofanya na usiku na muchana kwa jinsi usiku na muchana visikuwe kwa wakati wake,


ndivyo itakuwa kwa agano nililofanya na mutumishi wangu Daudi. Nilifanya agano na Daudi kwamba atakuwa na mumoja wa uzao wake wa kutawala pahali pake siku zote; vilevile kutakuwa makuhani wa ukoo wa Lawi watakaonitumikia siku zote.


Wakati huo nitawakusanya, na kuwafanya mujulikane na kusifiwa kati ya watu wote katika dunia, na kuwarudishia hali yenu njema, nanyi mutaona kwa macho yenu wenyewe. –Ni Yawe anayesema hivyo.


Muwafundishe kutii maneno yote niliyowaagiza. Na mujue kwamba mimi ni pamoja nanyi siku zote hata mwisho wa dunia.”


Lakini, kufuatana na ahadi ya Mungu, tunangojea kwamba kutakuwa mbingu mupya na dunia mupya, pahali haki itakapokuwa.


Kisha nikaona mbingu mupya na dunia mupya. Kwa sababu mbingu ya kwanza na dunia ya kwanza vilikuwa vimekwisha kutoweka, bahari nayo haikukuwa tena.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ