Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 66:20 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

20 Watawarudisha wandugu zenu wote kutoka katika mataifa yote kama matoleo yangu mimi Yawe. Watawaleta juu ya farasi, juu ya nyumbu, juu ya ngamia na ndani ya magari na juu ya vipoyi mpaka Yerusalema, kwenye mulima wangu mutakatifu. Watawaleta kama Waisraeli wanavyoleta sadaka ya unga katika chombo safi mpaka ndani ya nyumba yangu mimi Yawe.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 66:20
20 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Katika mulima mutakatifu wa Mungu hakutakuwa ubaya wala uharibifu. Maana kumujua Yawe kutaenea pote katika inchi, kama vile maji yanavyojaa katika bahari.


Katika siku zinazokuja, itatukia kwamba mulima wa nyumba ya Yawe utaimarishwa kupita milima yote, utainuliwa juu ya vilima vyote. Mataifa yote yatajaa kule,


watu wengi wataenda kule na kusema, Mukuje tupandie kwenye mulima wa Yawe, tuende kwenye nyumba ya Mungu wa Yakobo, apate kutufundisha njia zake, nasi tutafuata mapito yake. Maana sheria itakuja kutoka Sayuni; neno la Yawe kutoka Yerusalema.


Nitaiambia kaskazini: “Uwaache waondoke”, na kusini: “Usiwazuize! Muwarudishe watu kutoka mbali, kutoka kila pahali katika dunia.


Muondoke! Muondoke! Mutoke pale! Musiguse kitu chochote kichafu! Muondoke kule Babeli! Mujitakase, enyi munaobeba vyombo vya Yawe.


maana utapanuka kila upande; wazao wako watarizi mataifa, miji iliyokuwa ukiwa itajaa watu.


nitamupatia nafasi ya ukumbusho na ya sifa katika nyumba yangu na kuta zangu, nafasi bora kuliko kuwa na wana na wabinti. Nitamupatia jina la kukumbukwa siku zote na ambalo halitafutwa hata kidogo.


hao nitawaleta katika mulima wangu mutakatifu, na kuwafurahisha katika nyumba yangu ya maombi; sadaka zao na sadaka za kuteketezwa zitakubaliwa kwenye mazabahu yangu. Maana nyumba yangu itaitwa: Nyumba ya maombi kwa ajili ya watu wote.


Lakini nitafanya nini na ninyi munaoniacha mimi Yawe, musioujali Sayuni, mulima wangu mutakatifu, munaotolea miungu chakula na divai kusudi iwapatie bahati zuri.


Imbwa wa pori na kondoo watakula pamoja, simba watakula majani kama ngombe, lakini chakula cha nyoka kitakuwa mavumbi. Katika mulima wangu wote mutakatifu, hakuna atakayeumiza au kuharibu kitu. –Ni Yawe anayesema hivyo.


Zaidi ya hayo, atapiga mahema yake makubwa kati ya bahari na mulima mutukufu na mutakatifu. Lakini atakuwa amefikia ukomo wake, na hakutakuwa mutu yeyote wa kumusaidia.


Kutoka ngambo ya mito ya Kushi watu wangu wanaoniomba, wale ambao wametawanyika, wataniletea sadaka yangu.


wakamuletea Yawe matoleo yao: magari sita yaliyofunikwa na ngombe dume kumi na wawili, gari moja kwa kila viongozi wawili na ngombe dume mumoja kwa kila kiongozi. Kisha kuvitoa mbele ya hema takatifu,


kuwa mutumishi wa Yesu Kristo kwa watu wa mataifa mengine. Ninafanya kazi ya ukuhani ya kuhubiri Habari Njema ya Mungu, kusudi watu wa mataifa mengine wapate kuwa kama sadaka inayokubaliwa na Mungu na iliyotakaswa na Roho Mutakatifu.


Hata nikitoa maisha yangu kuwa sadaka pamoja na imani yenu inayokuwa sadaka mbele ya Mungu, mimi ninafurahi na kushiriki pamoja nanyi wote.


Nanyi vilevile, kama mawe yenye uzima mutumiwe kwa kujenga hekalu la kiroho. Na mule mutafanya kazi takatifu ya ukuhani kwa kutoa sadaka za kiroho zinazomupendeza Mungu kwa njia ya Yesu Kristo.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ