Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 66:19 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

19 Nitaweka kati yao kitambulisho cha uwezo wangu. Watakaookolewa kati yao nitawapeleka kwa watu wa mataifa kule Tarsisi, Puti, Ludi, inchi zenye wafundi wa kupiga upinde; watakwenda vilevile Tubali na Ugriki na katika visanga vya mbali ambapo watu hawajapata kusikia habari zangu wala kuuona utukufu wangu. Wale wajumbe wangu watautangaza utukufu wangu katika mataifa hayo.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 66:19
48 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Misiraimu alikuwa babu ya Waludi, Waanamu, Walehabi, Wanafutuhi,


Wana wa Yafeti walikuwa Gomeri, Magogi, Madayi, Yavani, Tubali, Meseki na Tirasi.


Wana wa Semu walikuwa Elamu, Asuri, Aripakisadi, Ludi na Aramu.


Wana wa Yavani walikuwa Elisa, Tarsisi, Kitimu na Rodanimu.


Mungu amuzidishe Yafeti, aishi katika hema za Semu; Kanana akuwe mutumwa wake.”


Wazao wa Misri ni: Waludi, Waanami, Walehabi, Wanafutuhi,


Wana wa Yavani walikuwa: Elisha, Tarsisi, Kitimu na Roda.


Mutangazie mataifa utukufu wake, muwaelezee watu wote matendo yake ya ajabu.


Wafalme wa Tarsisi na visiwa wamulipe kodi, wafalme wa Sheba na Seba wamuletee zawadi.


Naye atasimika bendera kuwaita mataifa, kuwakusanya Waisraeli waliozarauliwa, kuwaleta pamoja watu wa Yuda waliotawanywa, na kuwarudisha toka pembe ine za dunia.


Enyi wakaaji wote katika ulimwengu, nanyi munaojaza dunia! Bendera itakaposimikwa kwenye mulima, muangalie! Baragumu itakapopigwa, musikilize.


Wakati huo, Yawe wa majeshi ataletewa sadaka kutoka kwa watu warefu na wenye ngozi laini, watu wanaotisha kwa karibu na kwa mbali, taifa la watu wenye nguvu na ushindi, ambalo inchi yake imegawanywa na mito. Ataletewa sadaka hizo kwenye mulima Sayuni anapoabudiwa yeye Yawe wa majeshi.


juu ya mashua yote makubwa ya Tarsisi, na juu ya mashua yote mazuri.


Waliopotoka katika roho watapata maarifa na wenye kunungunika watakubali kufundishwa.


Wote wanaokaa katika inchi za mbali, wamutukuze na kumusifu Yawe.


Yeye hataregea wala kuchoka, mpaka atakapoimarisha sheria yangu katika dunia. Watu wa mbali wanangojea mafundisho yake.


Nitaiambia kaskazini: “Uwaache waondoke”, na kusini: “Usiwazuize! Muwarudishe watu kutoka mbali, kutoka kila pahali katika dunia.


Munisikilize, enyi inchi za mbali, Mutege sikio, enyi watu wa mbali! Yawe aliniita mbele sijazaliwa, alitaja jina langu nikiwa katika tumbo la mama yangu.


Watu wangu watarudia kutoka mbali, wengine kutoka kaskazini na magaribi, wengine kutoka upande wa kusini.


Bwana wetu Yawe anasema hivi: Nitasimika bendera kwa kuita mataifa; nitayaonyesha kitambulisho. Nayo yatawarudishia wana wenu wakiwabeba kwenye kifua, vilevile na wabinti zenu kwenye mabega.


Ukombozi wangu unakaribia upesi; wokovu nitakaoleta unaanza kutokea. Mimi mwenyewe nitayatawala mataifa. Wakaaji wa inchi za mbali wananingojea, wanaitegemea nguvu yangu.


Yawe ameonyesha nguvu yake tukufu, mbele ya mataifa yote. Atawaokoa watu wake, na ulimwengu wote utashuhudia.


Lakini sasa ameyashangaza mataifa mengi. Wafalme watapumbazika kwa sababu yake, maana wataona mambo ambayo hawajapata kuambiwa, na kufahamu mambo ambayo hawajapata kusikia.


Sasa utayaita mataifa usiyoyajua, watu wa mataifa yasiyokutambua watakuja mbio kwenu, kwa sababu yangu mimi Yawe, Mungu wako; kwa sababu yangu mimi Mutakatifu wa Israeli niliyekufanya wewe upate utukufu.


Ni mashua zinazotoka katika inchi za mbali, zikitanguliwa na mashua za Tarsisi. Zinawaleta watoto wako, pamoja na feza na zahabu yao, kwa sifa ya Yawe, Mungu wako, kwa sifa ya Mungu, Mutukufu wa Israeli, maana amewafanya mupate utukufu.


Enyi wakaaji wa Yerusalema, mutoke, mutoke inje ya muji, muwatayarishie njia watu wenu wanaorudia! Mujenge! Mujenge barabara na kuondoa mawe yote! Muweke bendera kuwa kitambulisho kwa ajili ya watu.


Yawe anasema; Nilikuwa tayari kujionyesha kwao wasiouliza habari zangu. Nilikuwa tayari kuwapokea wale wasionitafuta. Nililiambia taifa ambalo halikuomba kwa jina langu: Niko hapa! Niko hapa!


Musonge mbele, enyi farasi; mushambulie, enyi magari ya vita. Mashujaa wasonge mbele: watu wa Etiopia na Puti wanaoshika ngao, watu wa Ludi, wafundi wa kutumia pinde.


Watu kutoka Persia, Ludi na Puti walijiunga katika kundi lako la waaskari; walilundika ngao zao na kofia zao kwenye kambi zao za kiaskari. Waaskari hao walikupatia utukufu.


Watu wa Yavani, Tubali na Meseki, walifanya biashara nawe, wakakupatia watumwa na vifaa vya shaba wapate vitu vyako.


Watu wote waliofungamana na Wamisri, ni kusema watu wa Etiopia, Puti, Ludi, Uarabu yote na Libya wataangamia pamoja nao.


Mesaki na Tubali ziko huko. Makaburi ya watu wake wote yanazizunguka. Wote waliuawa katika vita, bila kujua Mungu. Walipokuwa wangali wanaishi, walieneza vitisho vyao katika inchi ya wanaokuwa wazima.


Bwana wetu Yawe akaniambia: Wewe mwanadamu! Toa unabii juu ya Gogi. Useme: Bwana wetu Yawe anasema hivi: Mimi nitapingana nawe Gogi mutawala mukubwa wa mataifa ya Meseki na Tubali.


Nitawasha moto juu ya inchi ya Magogi na juu ya wote wanaokaa salama katika inchi za kandokando ya bahari. Nao watatambua kwamba mimi ni Yawe.


Nyuma ya hayo, atageukia na kushambulia inchi nyingi za kandokando ya bahari na kuzishinda. Lakini jemadari mugeni atamushinda na kuyakomesha majivuno yake mwenyewe; kweli atamurudishia mufalme wa kaskazini majivuno yake mwenyewe.


Wao watamwogopa sana Yawe; ataiangamiza miungu yote ya dunia. Mataifa yote katika dunia yatamwabudu; kila taifa katika pahali pake.


Kutoka ngambo ya mito ya Kushi watu wangu wanaoniomba, wale ambao wametawanyika, wataniletea sadaka yangu.


Watu wa mataifa katika dunia yote tokea upande jua linapopanda mpaka upande jua linaposhuka wanalitukuza jina langu. Kila pahali wananifukizia ubani na kunitolea sadaka zinazokubaliwa; maana jina langu linatukuzwa kati yao.


Basi muwaendee watu wa mataifa yote kusudi wapate kuwa wanafunzi wangu, mukiwabatiza kwa jina la Baba, la Mwana na la Roho Mutakatifu.


Kisha akawaambia: “Mwende katika dunia yote na kuhubiri Habari Njema kwa kila mutu.


Simeoni akawabariki na kumwambia Maria, mama yake: “Mutoto huyu amezaliwa kwa sababu ya kuwaangusha na kuwasimamisha watu wengi katika Israeli. Naye atakuwa kitambulisho kutoka kwa Mungu watu watakachokipinga,


kama vile inavyoandikwa katika Maandiko Matakatifu: “Wale ambao hawajaambiwa bado habari zake, watamwona. Wale hawajazielezwa bado, watazifahamu.”


Mimi ni mudogo kuliko watu wote wa Mungu, lakini Mungu amenijalia neema ya kutangaza kwa watu wa mataifa mengine Habari Njema ya baraka za Kristo zisizoweza kuhesabiwa.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ