Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 66:13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

13 Kama vile mama anavyomufariji mwana wake, vilevile nami nitawafariji; mutafarijiwa katika Yerusalema.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 66:13
13 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Ulimi wangu ukuwe muzito, kama nisipokukumbuka wewe, ee Yerusalema, nisipokufurahia kuliko furaha yangu kubwa!


Mahangaiko ya moyo wangu yanapozidi, wewe unanifariji na kunifurahisha.


Siku hiyo mutasema: Ninakushukuru, ee Yawe, maana ingawa ulinikasirikia, hasira yako imetoweka, nawe umenifariji.


Mungu wenu anasema hivi: Muwafariji watu wangu. Muende kuwafariji.


Museme na watu wa Yerusalema kwa upole, muwaambie kwamba utumwa wao umekwisha, wamesamehewa uovu wao. Yawe amewaazibu mara mbili kwa sababu ya zambi zao zote.


Muimbe kwa furaha, enyi mbingu! Ushangilie ewe dunia, Enyi milima, mulalamike kwa furaha, maana Yawe amewafariji watu wake, anawaonea huruma watu wake wanaoteseka.


Yawe anasema hivi: Mimi, kweli mimi, ndiye ninayekufariji. Kwa nini wewe unamwogopa mutu ambaye ni wa kufa, mwanadamu ambaye anatoweka kama majani?


Mimi Yawe nitaufariji Sayuni, nitatengeneza pahali pake pote palipoharibika. Nitazifanya mbuga zake kama shamba la Edeni, jangwa yake kama bustani ya Yawe. Ndani yake kutapatikana furaha na shangwe, na nyimbo za shukrani zitasikilika humo.


Mushangilie na kufurahi pamoja na Yerusalema, enyi munaoupenda! Mushangilie pamoja nao, enyi wote mulioulilia!


Asifiwe Mungu na Baba ya Bwana wetu Yesu Kristo, Baba mwenye kujaa huruma na Mungu anayefariji katika mambo yote!


Yeye anatufariji katika taabu yetu yote, kusudi tupate kuwafariji wale wanaokuwa katika taabu yoyote kwa kuwaletea faraja tuliyopokea kutoka kwa Mungu.


ijapokuwa sisi ni mitume wa Kristo, tungeweza kudai mambo fulani kwenu. Lakini sisi tulionyesha upole kati yenu kama vile mama anavyosumbuka kwa ajili ya watoto wake.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ