Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 65:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Nitawajalia watu wa Yakobo, na Yuda nitamujalia watakaorizi milima yangu; wachaguliwa wangu watairizi, watumishi wangu watakaa kule.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 65:9
25 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Itakuja siku wazao wa Yakobo watatoa mizizi; watu wa Israeli watachanua na kuchipuka, na kuijaza dunia yote kwa matunda.


Enyi watu wa Sayuni, enyi watu wa Yerusalema, hakika ninyi hamutaomboleza tena. Kweli Mungu atawahurumia; mara tu atakaposikia kilio chenu atawaitikia.


Watu wangu watakaa katika makao ya amani, katika pahali penye usalama na nafasi yenye utulivu.


Mimi sikusema kwa siri, wala katika inchi yenye giza. Mimi sikuwaambia wazao wa Yakobo wanitafute pahali kusipokuwa kitu. Mimi Yawe ninasema ukweli, maneno yangu ni ya kuaminika.


Lakini wazao wa Israeli watapata ushindi toka kwa Yawe na kufurahi.


Yawe anasema hivi: Wakati uliofaa nilijibu maombi yako; wakati wa wokovu nilikusaidia. Nimekuweka na kukufanya ukuwe kiungo cha agano langu na mataifa yote: utatengeneza inchi na kurudisha tena inchi hiyo iliyoharibika.


Mutakapolia kwa kuomba musaada, basi ile lundo ya sanamu zenu iwaokoe! Upepo utavipeperushia mbali; pumzi itavitupilia mbali. Lakini watakaotafuta kimbilio kwangu, watarizi inchi, mulima wangu mutakatifu utakuwa mali yao.


Watu wako wote watakuwa wa haki, nao watarizi inchi milele. Hao ni chipukizi nililopanda mimi, kazi ya mikono yangu kwa ajili ya utukufu wangu.


Wale niliowachagua nitawapa jina jipya. Lakini ninyi jina lenu watalitumia kwa kulaani; watasema: Bwana wetu Yawe awaue.


Hawatajenga nyumba na watu wengine wakae ndani yake, wala kulima chakula kikuliwe na watu wengine. Maana watu wangu niliowachagua wataishi maisha marefu kama miti; wachaguliwa wangu watafurahia matunda ya jasho lao.


Nitawaondoa ninyi katika kila taifa na kuwakusanya kutoka inchi zote za kigeni; nitawarudisha katika inchi yenu wenyewe.


Wakati huo nitawakusanya, na kuwafanya mujulikane na kusifiwa kati ya watu wote katika dunia, na kuwarudishia hali yenu njema, nanyi mutaona kwa macho yenu wenyewe. –Ni Yawe anayesema hivyo.


Na kama Mungu asingepunguza siku zile za mateso, hakuna hata mutu mumoja angeponyoka kufa. Lakini kwa ajili ya watu wake aliowachagua, yeye atazipunguza.


Wayuda wamegeuka waadui za Mungu kwa sababu ya kukataa Habari Njema, na jambo hilo limekuwa faida kwenu ninyi watu wa mataifa mengine. Lakini wao ni wapendwa wake kufuatana na vile wamechaguliwa naye, kwa njia ya babu zao.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ