Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 65:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Mujue kwamba mambo hayo yameandikwa mbele yangu, sitanyamaza lakini nitawalipiza; nitawalipa sawa inavyostahili.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 65:6
22 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wengine walipumbazika kwa sababu ya zambi zao, waliteseka kwa sababu ya uovu wao;


Yawe akumbuke uovu wa babu zake, zambi za mama yake zisifutwe hata kidogo!


Umefanya hayo yote nami nimenyamaza. Unazani kwamba mimi ni kama wewe? Lakini sasa nitakukaripia, nitakugombeza waziwazi.


Mungu wetu anakuja, lakini si kimyakimya: moto wenye kuteketeza unamutangulia, na zoruba kali inamuzunguka.


Ee Mungu, uwalipe kwa kadiri ya uovu wao, uwaangushe hao waovu kwa hasira yako.


Ee Bwana, uwalipize mataifa jirani mara saba kwa ajili ya matusi waliyokutukana.


Kisha Yawe akamwambia Musa: “Uandike jambo hili katika kitabu, likuwe ukumbusho. Tena umwambie Yoshua kwamba nitawafuta kabisa Waamaleki katika dunia.”


Maana Yawe anakuja kutoka kwake juu, kutoka makao yake huko mbinguni; kuwaazibu wakaaji wa dunia kwa uovu wao. Nayo dunia haitaficha tena wale waliouawa, lakini itaufichua umwagaji wa damu wote.


Lakini ole kwao watu waovu! Mambo yatawaendekea vibaya, maana yale waliyotenda yatawapata wao wenyewe.


Yawe anasema hivi: Kwa muda murefu sasa nimenyamaza, nimekaa kimya na kujizuiza; lakini sasa nitalia kama mwanamuke wakati wa kuzaa, anayeugua pamoja na kupumua kwa nguvu.


Atawaazibu waadui kadiri ya matendo yao, kasirani yake na kisasi vitawapata waadui zake; atawaazibu hata wakaaji wa inchi za mbali.


Musikilize: makelele kutoka katika muji, sauti kutoka katika hekalu! Hiyo ni sauti ya Yawe akiwaazibu waadui zake!


Nitalipiza kisasi mara mbili zaidi juu ya zambi zao na makosa yao, kwa sababu wameichafua inchi yangu na mizoga ya miungu yao yenye kuchukiza, wameijaza inchi yangu na hayo machukizo yao. –Ni ujumbe wa Yawe.


Lakini hao ambao moyo wao umeambatana na vitu vichafu na machukizo yao, nitawaazibu kadiri ya mienendo yao. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.


Kwa hiyo nimewamwangia kasirani yangu na kwa moto wa hasira yangu nimewateketeza kulingana na matendo yao. –Ndivyo anavyosema Bwana wetu Yawe.


Kwa upande wangu, sitawaachilia wala kuwahurumia; nitawatendea kufuatana na matendo yao.


Jua litatiwa giza, na mwezi utakuwa kama damu, mbele ya kutimia kwa siku ya Yawe, siku inayokuwa kubwa na ya kutisha.


Halafu watu wanaomutii Yawe walizungumuza wao kwa wao, naye Yawe akasikia mazungumuzo yao. Mbele yake kukawekwa kitabu ambamo uliandikwa ukumbusho wa wale wanaomutii na kumuheshimu.


Muwape wengine, na Mungu atawapa ninyi. Mutapokea kipimo kikubwa kilichojaa zaidi. Kwa maana mutapimiwa na kipimo kile munachotumia kwa wengine.”


Sina njia ya kuwaazibu? Silaha zangu ziko katika mukono wangu.


Nikaona wale waliokufa, wakubwa na wadogo wakisimama mbele ya kile kiti cha kifalme. Vitabu vikafunguliwa na kitabu kingine kikafunguliwa ndicho kitabu cha uzima. Wale waliokufa wakahukumiwa kufuatana na matendo yao sawa vile ilivyoandikwa katika vitabu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ